Wananchi katika vijiji
vya mpanga na Mombo tarafa ya mambwenkoswe wilayani kalambo mkoani Rukwa wameiomba
serikali kuwapatia misaada ya kibinadamu kutokana na nyumba zao zipatazo 20
kubomoka kutokana na mvua kubwa iliokuwa imeambatana na upepo mkali kunyesha na
kubasababisha baadhi yao kukosa makazi
na kujihifadhi kwa majirani.
Wananchi hao kwa nyakati
tofauti wamesema mvua hiyo imeharibu makazi yao kwa kuezua mapaa na kubomoa nyumba
na kueleza kuwa mvua hiyo ilinyesha ikiwa imeambatana na upepo mkali.
Wamesema kufuatia
hali hiyo walitoa taarifa kweye uongozi wa kijiji na kata ambao ulifikika eneo
la tukio kisha kutoa taarifa wilayani ambao ulifika na kutembelea maeneo yote yaliokuwa
yameathirika.
Afisa tarafa ya
Mambwenkoswe Mpapalika Mfaume, amekili kuwepo kwa adha hiyo na kusema mvua hiyo
ilinyesha na kubomoa nyumba (8) katika kijiji cha Mombo kata ya Legezamwendo na
yumba(12) katika kijiji cha Mpanga na kusema mpaka sasa wanaendelea na jitihada za kuwasaidia
wananchi waliokumbwa na kadhia hiyo kwa kuwapatia
misaada ya kibinadamu pamoja na kusaidia
kuzinyenyua nyumba zilizokuwa zimeathirika na kadhia hiyo.
Amesema wameomba
sementi kupitia mfuko wa jimbo ili kusaidia ujenzi wa zahanati ya kijiji cha
Mpanga ambayo imeezuliwa kutokana na mvua hiyo na kusema sehemu zilizo athirika
kwa kiasi kikubwa ni nyumba za wananchi
, Kanisa na Zahanati moja.
Comments
Post a Comment