Rais Trump amesema "amemfuta kazi " mkuu wa usalama wa
mtandao na shirika la usalama wa miundo mbinu ya uchaguzi (Cisa) Chris Krebs
kwa taarifa zake "zisizo sahihi kwa kiwango cha juu " kuhusu maadili
ya kura.
Bwana Trump amekataa kukubali kushindwa katika uchaguzi wa
Marekani, akitoa madai yasiyo na ushahidi ya wizi "mkubwa " wa kura
Maafisa wa uchaguzi wanasema kura ya mwaka huu ilikuwa "moja ya kura salama zaidi " katika historia ya Marekani.
Wiki iliyopita Rais Trump alimfuta kazi waziri wa ulinzi Mark
Esper, huku kukiwa na ripoti kwamba alikuwa na wasiwasi juu ya utiifu wa mkuu
huyo wa Pentagon.
Comments
Post a Comment