Trump Amfuta Kazi Afisa Wa Uchaguzi Aliyepinga Madai Yake

 

Rais Trump amesema "amemfuta kazi " mkuu wa usalama wa mtandao na shirika la usalama wa miundo mbinu ya uchaguzi (Cisa) Chris Krebs kwa taarifa zake "zisizo sahihi kwa kiwango cha juu " kuhusu maadili ya kura.

 

Bwana Trump amekataa kukubali kushindwa katika uchaguzi wa Marekani, akitoa madai yasiyo na ushahidi ya wizi "mkubwa " wa kura

Maafisa wa uchaguzi wanasema kura ya mwaka huu ilikuwa "moja ya kura salama zaidi " katika historia ya Marekani.

Wiki iliyopita Rais Trump alimfuta kazi waziri wa ulinzi Mark Esper, huku kukiwa na ripoti kwamba alikuwa na wasiwasi juu ya utiifu wa mkuu huyo wa Pentagon.

Comments