Rais wa Tanzania, John Magufuli amefungua Bunge la 12 mjini
Dodoma na kulihutubia Bunge hii leo.
Akiwahutubia wabunge hii leo, Magufuli ametoa dira ya serikali
yake baada ya kumaliza awamu ya kwanza.
Rais Magufuli amesema mambo muhimu anayoyapa kipaumbele katika
miaka mitano ijayo ni;
Kuendelea kulinda na kudumisha tunu za taifa, yaani amani, umoja
na mshikamano , uhuru wa nchi, Muungano na mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
'' Katika hilo ninaahidi kushirikiana kwa ukaribu sana na Rais
mpya wa Zanzibar, Dkt Hussein Mwinyi. Kamwe hatutakuwa na mzaha na yeyote
mwenye kutaka kuhatarisha amani ya nchi yetu. Mwenye nia ya kuvuruga umoja na
mshikamano wetu, pia mwenye kutaka kutishia uhuru wetu, Muungano pamoja na
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar." alisema Rais Magufuli.
Rais Magufuli amemuahidi Dkt Hussein Mwinyi kuwa katika kipindi
cha miaka mitano ijayo serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania itafanya
kazi kwa karibu sana na Serikali ya Zanzibar ili kuleta maendeleo kwa pande
zote mbili za Muungano.
Comments
Post a Comment