MKUU
wa wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa Calorus Misungwi ametoa siku tatu kwa
viongozi wa serikali za vijiji vitatu vya kata ya Kisumba kuhamasisha wananchi kujitokeza
kwenye shughuli za maendeleo ya ujenzi wa bweni la wanafunzi wa shule ya
sekondari Chisenga.
Ameyasema
hayo baada ya kutembelea ujenzi wa miradi ya maendeleo katika kata hiyo na kubaini
kusua sua kwa ujenzi huo kutokana na wananchi pamoja na viongozi wa serikali za
vijiji hivyo kususia ujenzi huo kwa madai ya fedha zilizoletwa na serikali
zilikuwa kwa ajili ya malipo ya vibarua na mafundi.
Kufuatia hali hiyo akawaagiza wenyeviti wa vijiji
hivyo pamoja na watendaji kufika ofisini kwake na kusisitiza watendaji
kuhakikisha wanawaweka ndani watu wote wanaogoma kushiriki kwenye shughuli za
maendeleo.
Kaimu mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo
Erick Kayombo, amesema fedha zote zinazotolewa kwenye miradi hiyo ni kwaajili ya
ujenzi, na kazi zingine zinazobakia zinatakiwa
kufanywa na wananchi.
“Shughuli
zote ndogo ndogo katika utekelezaji wa miradi hii zinatakiwa kufanywa na
wananchi mfano ubebaji mchanga, kubeba mawe na kuchimba misingi zote hizo kwa ujumla
wake zinafanywa na wananchi,
Aidha
aliwataka wananchi kuendelea kushiriki kwenye shughuli za maendeleo kwa lengo
la kuwezesha miradi hiyo kukamilika kwa haraka.
Hivi
karibuni serikali ilitoa fedha kiasi cha shilingi million 38.45 kwa ajili ya
ujenzi wa bweni la wanafunzi katika shule ya sekondari Chisenga na ujenzi wa
vyoo katika shule ya msingi Kasote.
Comments
Post a Comment