Zaidi Ya Wananchi 1700 Wajitokeza Kufanya Usahili Wa Usimamizi Wa Vituo Vya Uchaguzi’’kalambo’’


Na Baraka lusajo- Kalambo

Imeelezwa kuwa kufuata misingi ya sheria, taratibu na kanuni zinazo tawala suala zima la uchaguzi wa viongozi ni nyenzo na nguzo muhimu ya amani, utulivu na ukuaji wa uchumi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na taifa lao.

Wakieleza kwa nyakati tofauti, watendaji wa uchaguzi ngazi ya vituo na jimbo waliojitokeza kwa wingi kwenye zoezi la usaili lililofanyika kwenye shule ya wasichana ya Matai Wilayani Kalambo mkoani Rukwa, wamesema wamefurahishwa na utaratibu huo mpya kwani unalenga kupata wasimamizi wenye weledi ili zoezi la uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani linalo tarajiwa kufanyika tarehe 28 oktoba 2020 lifanyike kwa mafanikio makubwa huku uhuru na haki vikitamalaki nchini kote na kuivusha nchi ikiwa salama.

Cosmasi Mbawala ambae  ni afisa uchaguzi msaidizi jimbo la Kalambo , amesema  zaidi ya watu (1700) wamejitokeza katika zoezi la usaili ambalo limefanyika katika maeneo tofauti ya wilaya hiyo na kusema  mahitaji ni 1376 .

Hivi karibuni, Kamishina wa uchaguzi taifa balozi Omar Ramadhani Mapuri akiwa kwenye kikao na wadau wa uchaguzi mkoani Rukwa alisisitiza umuhimu wa vyama vya siasa na wagombea kuzingatia maadili katika kampeni zao na kuwa taka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 28 oktoba kwani maandalizi yote yamekamilika.

“wakati tume inaendelea kuratibu, kusimamia na kuendesha uchaguzi huu kwa kutumia sheria za uchaguzi, vyama vya sisa wagombea na wananchi wanakumbushwa kuwa katika kipindi hiki, sheria nyingine za nchi hazijasimama hivyo wajihadhari na vitendo vya matamshi ambayo yanaweza kusababisha vurugu kwa kisingizio cha uchaguzi. Alisema balozi Mapuli.


Comments