Watoto Wa Kike Waomba Mabweni Mashuleni kujengwa




Na mwandishi wetu kalambodc.

WATOTO wameomba kuwepo na Mabweni katika shule za Sekondari ili kuondoa uwezekano wa Watoto hao kwenda kupanga vyumba mjini wawapo shuleni ili kuweza kuondokana na mimba za utotoni.

Ombi hilo limetolewa jana na Wanafunzi wa shule za Sekondari za Mashete,Mtenga,Milundikwa,Mkwamba,Isale,Mkangale,Nkomolo na Nkasi sekondari kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto  wa kike ambapo wamedai kuwa kitendo cha wao kupanga vyumba mjini ni kichocheo kikubwa cha wao kupata vishawishi vinavyopelekea kupata mimba na kukatishwa masomo yao.


Wakizungumza kwenye mdahalo Maalumu ulioandaliwa na shirika lisilokuwa la kiserikali la Plan International  juu ya Matumizi ya mitandao ya kijamii kama ikitumika vibaya inaweza kuwapa madhara ya kupata mimba na ndoa za utotoni  bila yao kutegemea walidai kuwa ni kweli lakini kubwa linalowasumbua wao kama Watoto wa kike ni kukaa mitaani badala bwenini ambako kuna uangalizi mkubwa.

Akizungumza kwenye mdahalo huo  Adolphina Kapembwa Mwanafunzi wa shule ya sekondari Mkangale alidai kuwa licha ya mitandao ya kijamii kuwa na changamoto kwao,lakini kubwa ni la kukosekana kwa Mabweni ya kutosha mashuleni inayopelekea wengi wao kwenda kupannga vyumba mitaani ambako ukutana na vishawishi vingi ambavyo ukwamisha ndoto zao walizojiwekea katika maisha yao.

Hivyo aliwaomba Wazazi wao,serikali na Wadau wengine kuliona jambo hilo kuwa ni la msingi kwa kuhakikisha kuwa katika shule zote za Sekondari  yanajengwa Mabweni ya kutosha kuwawezesha Watoto wote hasa wa kike wanaishi kwenye Mabweni kuliko na uangalizi mkubwa ukilinganisha na mitaani kwenye vishawishi vingi.

Benezeth Mtuka kwa upande wake alisema kuwa Mitandao ya kijamii ni muhimu kwa maendeleo lakini pale inapotumika vibaya ina madhara makubwa hasa kwa Watoto wa kike bali kinachotakiwa ni Wao wenyewe Watoto kujitambua kuwa wao ni nani? Na lengo lao nini wawapo shule na kuwa hilo likiwezekana mimba na ndoa za utotoni zitatoweka kabisa kwa Watoto walio mashuleni.

Mwakilishi wa dawati la  jinsia na Watoto Atupele Hance alisema kuwa   changamoto kubwa wanayoipata jeshi la Polisi ni kupata ushahidi dhidi ya vitendo hivyo na kuwa kama Watoto wenyewe wangekua Wawazi vitendo hivyo vya  mimba za Utotoni ingekua ni ndoto.

Alisema kuwa kama Wasichana wangekua wanatoa taarifa pale wanapotongozwa ingeasaidia sana kuwawekea ulinzi lakini kitendo cha kukaa kimya kinawapa nguvu Wanaume cha kuendelea kuwarubuni na mwisho wa siku wanaingia mitegoni.

Meneja miradi wa Plan International  Williamu Mtukananje alisema kuwa shirika lake kwa kushirikiana na serikali wamekua katika vita hiyo kubwa ya kukabiliana na mimba za Utotoni na kuwa hivi sasa vita hiyo imeeleweka kwa jamii bali kinachotakiwa sasa ni ushirikiano toka kwa wazazi kwa maana ndiyo wamekua wakiharibu kesi hizo pindi ziendapo mahakamani

mwisho

 


Comments