Na Mwandishi wetu kalambodc.
Wafanyakazi wakiwemo watumishi wa umma na mashirika binafus mkoani Rukwa wametakiwa kuendelea kumwenzi hayati baba wa taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kuenzi na kudumisha misingi ya uwajibikaji alio uacha enzi za uhai wake.
Katika
kumwenzi hayati baba wa taifa walimu Julius Kambarage Nyerere, Baraza la la wafanyakazi
wilayani Kalambo limeketi katika kikao cha pamoja na kusisitiza wafanyakazi
kuendeleza misingi ya uwajibikaji alioiacha baba wa taifa enzi za uhai wake.
Dastani
Mshanga ambae ni kaimu katibu wa chama cha walimu CWT mkoa wa Rukwa, amesema mwalimu
nyerere aliacha misingi mizuri ambayo kila mfanyakazi anapaswa
kuitekeleza kwa vitendo.
Raphael
Mikoma ambae ni mwenyekiti TUGE wilayani Kalambo,alisema watamkumbuka mwalimu Nyerere
kwa kuhamasisha uwajibikaji na uzalendo kwa
watanzania na kusema ili kumwezi kila mtumishi anawajibu wa kuyaenzi
matendo yake kwa vitendo.
Mwenyekiti
wa baraza la wafanyakazi wilayani humo ambae pia ni Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri
hiyo Msongela Palela, alitumia fulsa hiyo kuwasihi na kuwahimiza wafanyakazi kuhamasisha
wananchi kujenga nyumba bora za watumishi ili serikali iweze kumalizia sehemu
inayobakia.
Comments
Post a Comment