Wananchi katika
Kata za Lyowa na Matai wilayani Kalambo mkoani Rukwa wamelaani vikali kitendo
cha mwamke mmoja ambae hakufahamika jina wala makazi yake kuuwawa kisha mwili
wake kutupwa kwenye mitalo ya maji ya mto Chimilango katika mtaa wa Keleni.
Wakazi maeneo
hayo wamesema mwili huo
ulikutwa kwenye mtalo wa maji yanayotumika kumwagilia Bustani za mboga mboga katika mtaa wa Keleni wilayani humo,
wamesema waliugundua mwili huo wakati wakisafisha mitalo hiyo.
Mwenyekiti wa mtaa
huo Linus Mawela, amesema mwili huo uligundulika wakati watu wakisafisha
vichaka kwenye mitalo hiyo na kusema baada ya kuona mifupa waliamua kutoa
taarifa kwenye uongozi wa kijiji ambao ulitoa taarifa polisi.
Amesema jeshi la polisi
lilifika eneo la tukio na kuwaruhusu wananchi kufanya madhishi pembezoni na mitalo hiyo, kwani
mwili huo ulikuwa haujagundulika kutokana na kuharibika vibaya.
Mtendaji wa kijiji
hicho Muhamed Rajabu, amesema mwili huo haujafahamika na kusema mwili huo ulikutwa katika maeneo ya bustani
ambako kuna mitalo ya kupitisha maji kwa ajili ya umwagiliaji.
Mganga mfawidhi wa
kituo cha afya Matai Dr.Edwini Mlingi ,amesema katika uchunguzi waharaka ilibainika kuwa marehemu
alikuwa ni wa kike na mwili wake unakadiliwa kuwa kwenye maji kwa zaidi ya miezi mitatu.
Comments
Post a Comment