Rc Wangabo Kupeleka Takukuru Faili La Ujenzi Wa Hosptali Ya Wilaya’’Nkasi’’



Na Israel Mwaisaka,Nkasi

MKUU wa mkoa Rukwa Joakhimu Wangambo amesema kuwa ataipeleka TAKUKURU kuchunguza matumizi ya fedha Tshs,Mil.300 zilizotumika kujengea hospitali ya wilaya Nkasi.

Akizungumza jana baada ya ukaguzi wa ujenzi wa hospitali ya wilaya mkuu huyo wa mkoa alidai kuwa haoni sababu ya hospitali hiyo kuchelewa kukamilika wakati fedha zimetolewa na serikali ukilinganisha na kasi iliyokuwepo awali.

Hilo lilikuja baada ya mkuu wa wilaya Nkasi Said Mtanda kumweleza mkuu wa mkoa kuwa hajalidhishwa na namna ambavyo halmashauri wamezisimamia fedha kiasi cha Tshs,Mil.300 katika kukamilisha ujenzi kwenye hospitali hiyo na haijakamilika na kuuomba mkoa kuingilia hari hiyo.

Mkuu wa mkoa kwa upande wake aliamua kuwakabidhi TAKUKURU kufanya uchunguzi wa jambo hilo na kuwa matokeo ya uchunguzi huo yatafanyiwa kazi.

Kufuatia hari hiyo mkuu wa mkoa Wangabo alitoa siku 14 kwa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya Nkasi Missana Kwangula kurekebisha kasoro hizo zilizojitokeza na kuwa baada ya muda huo atarudi kuona maagizo hayo yametekelezwa kwa kiasi gani.

Sambamba na hilo mkuu huyo wa mkoa amemtaka mkandarasi wa ujenzi wa Tanki la maji mjini Namanyere kuhakikisha kuwa ujenzi wake unakamilika kwa muda uliopangwa.

Alisema kuwa anasikitishwa na kasi ndogo ya ujenzi wa tanki hilo na kuwa kwa mujibu wa mkataba ilibidi ujenzi wa Tanki hilo uwe umekamilika na jamii kuendelea kupata huduma ya maji

Kaimu meneja wa SUASA Emmanuel Mashauri alisema kuwa ujenzi wa tanki hilo mpaka sasa umefikia asilimia 92 na kuwa siku chache zijazo kazi hiyo itakua imekamilika na litaanza kutoa huduma ya maji kwa jamii

Alisema kuwa hadi sasa hari ya upatikanaji wa maji katika mji wa Namanyere ni asilimia 16 tu na kuwa mradi huo utaongeza wigo mpana wa upatikanaji wa maji.

Mwisho 

 

Comments