Charles Ndereyehe: Mshukiwa wa mauaji ya kimbari ya Rwanda atiwa nguvuni na kuachiliwa Uholanzi

 


Mtuhumiwa wa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 Charles Ntahontuye Ndereyehe amekamatwa kutoka nyumbani kwake mjini Amsterdam nchini Uholanzi, kabla ya kuachiliwa kimesema chama chake.

 

Bwana Ndereyehe ,70, ni mjumbe maarufu wa FDU na mkosoaji wa serikali ya Rwanda. Wakati wa mauaji ya kimbari alikuwa ni Mkuu wa taasisi ya utafiti wa kilimo ya serikali iliyopo kusini mwa Rwanda.

Polisi bado hawajatoa kauli yoyote juu ya kukamatwa kwa Bwana Ndereyehe, ambaye amekuwa akiishi nchini Uholanzi kwa miaka zaidi ya 15.

Ndereyehe anashukiwa kuwa mmoja wa watu waliopanga mauaji ya mwaka 1994 na kesi yake ilisikilizwa bila mtuhumiwa huyo kuwepo katika mahakama ya kijadi maarufu Gacaca mwaka 2008.

Mnamo mwaka 2010, Rwanda ilitoa kibali cha kimataifa cha kumkamata na alikuwa katika orodha ya watu waliokuwa wakisakwa na polisi wa kimataifa Interpol.

Comments