Watu WawiliWafariki Dunia Kwa Wivu Wa Kimapenzi

 

katika  picha ni baadhi  ya wananchi  wakiwa   eneo  la madhishi

 Wananchi wa kijiji cha Mbuluma wilayani Kalambo mkoani Rukwa wamemuua kwa kumchoma moto Amosi Kapufi miaka 22 mkazi wa kijiji cha Myunga baada ya kumchoma kisu mtoto wa dada yake aliefahamika kwa jina la Catherin Kakusu na kufariki dunia papo hapo kutokana na wivu wa kimapenzi.

Imedaiwa kuwa marehemu kabla ya kifo chake alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na binti huyo ambae alikuwa akiishi katika kata jirani  na maeneo anayoishi wilayani humo.

Kwa mujibu wa mzazi wa kijana huyo, Bosko Kapufi, amebainisha kuwa kabla ya kifo chake, marehemu alikuwa ameelekea kwenye kata ya Mbuluma kwa lengo la  kuwaona ndugu zake, ambapo baada ya kukutana na binti huyo alianzisha vurugu  na kumchoma kisu binti huyo katika  sehemu za tumbo na shingoni na kufariki dunia.

Amesema kufuatia tukio hilo wananchi kutoka sehemu mbalimbali walikusanyika  kisha kumpiga kijana huyo .

“Kifo cha kijana wangu kimenisikitisha sana kwani kijana huyu alikuwa mwaka wa kwanza katika chuo kikuu cha Sauti hivyo sote tumepata hasara kubwa sisi kama wazazi lakini pia serikali”. Alisema  Kapufi

Mkuu wa wilaya ya Kalambo Julieth Binyura , alikiri wazi  kutokea tukio hilo na  kusema tukio hilo lilitokea  baada  ya  watu  hao kutofautiana na kuwasihi wananchi  kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi .

“Tukio hili limetusikitisha sana wananchi wa  Kalambo kwani kitendo cha kufanya mauaji ni kosa, hivyo niwatake wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria  mkononi na badala yake kunapotokea tatizo waende kwenye uongozi husika”. Alisisitiza Binyura.


Comments