MASHAURI YOTE YA MAHAKAMA KUTUMWA KWA NJIA YA SIMU




Wananchi mkoani Rukwa wameiomba serikali  kuweka utaratibu maalumu ambao utawawezesha kutoa ushahidi mahakamani kwa kujirekodi na kutuma video pamoja na vinasa sauti mahakani badala ya kuapa kwa lengo la kusadia watu kupata haka zao kwa wakati.


Wakiongea wakati wa maadhimisho ya siku ya sheria yaliyofanyika wilayani  Kalambo, walisema serikali haina budi kuziwezesha mahakama kwa kuruhusu  watu  kutuma  video  pamoja na vinasa  sauti na kutumika kama ushahidi wakati  wa uendeshaji kesi mahakamani.

Hakimu wa mahakama ya wilaya ya Kalambo Ramadhani Rugemalira ambae alikuwa mgeni rasm kwenye madhimisho  hayo, alisema kwa sasa mashauri yote  yatatumwa kwa njia ya simu.

‘’katika kupunguza  gharama za mashauri kwa  wadau ,mahakama imeanzisha huduma ya mahakama inayotembelea {mobile court }alisema Rugemalila.

Alisema hali  kadhalika kwa  sasa mahakama inatumia  mitambo  ya  kielektroiniki {viedo conferece  facility }kuendesha mashauri mbalimbali  kwa baadhi  ya  maeneo  hapa  nchini.

Alisema  mahakama  ya  Tanzania  katika   kuhakikisha  mashauri  ya  biashara   na uwekezaji  yanaisha kwa  haraka ,msisitizo  mkubwa umewekwa kwenye utatuzi wa mashauri  kwanjia  ya  usuluhishi {Altenative  dispute resolusion }

Alisema  kwa  upande  wa  mahakama  ya  mwanzo mashauri yatatakiwa  kumalizika  ndani  ya  miezi  sita  ,mahakama za hakimu  mkazi  miezi kumi na  mbili  kwa  mwaka  mara  moja .

Mkuu  wa  wilaya  ya  kalambo Julieth Binyura aliwataka  wananchi kujenga  mazoea  ya  kufika mahakamani  kutoa  ushahidi.

‘’wananchi pia  ni  wadau  muhimu  katika  kuhakikisha kunakuwepo  namazingira wezeshi ya  biashara na uwekezaji.kunapokuwa  na shauri lolote mahakamani  zikiwemo  kesi za biashara  na uwekezaji  ni jukumu  la wananchi kufika mahakani  kutoa  ushahidi ili  kesi ziweze kufikia maamuzi sahihi na ya haki kwa  wakati.’’Alisema Binyura.

Madhimisho   ya  sheria  hufanyika tarehe 6 ya kila  mwaka  na  kwa mwaka  huu yalikuwa  na kauli  mbiu  isemayo‘’Uwekezaji na biashara,Wajibu wa mahakama  na wadau  kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji’’


Comments