katika picha ni katibu tawala wilayani kalambo Frank Sichalwe ,akiongea na viongozi katika tarafa ya kasanga |
BAADHI
ya wazazi wilayani Kalambo mkoani Rukwa wameiomba serikali kuanzisha mpango maalumu
wa kuwapima ujauzito wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kila baada
ya miezi mitatu kama ilivyo katika maeneo mengine ya mkoa huo ili
kuwabaini walioanza kujihusisha na vitendo vya kimahusiano ya kingono na wanaume katika umri mdogo
Ombi
hilo walilitoa kwa nyakati tofauti wakati wakizungumza na mwandishi wa habari hizi,muda
mfupi baada ya kikao kazi kilichowakutanisha Katibu tawala wa wilaya hiyo
Frank Sichalwe pamoja na viongozi wa serikali za vijiji, kata pamoja na maofisa
elimu kata waliopo katika maeneo ya mwambao wa ziwa Tanganyika.
Mmoja
wa wazazi hao aliyejitambulisha kwa jina la Getruda Siwale mkazi wa kijiji cha
Kasanga, alisema kuwa imefika wakati kwa serikali kutumia njia hiyo kwani
tatizo la mimba za utotoni pamoja na kwa wanafunzi limekuwa ni changamoto kubwa
hivyo ni lazima zibuniwe mbinu zitakazo sababisha wanafunzi hao kuogopa
kushiriki ngono.
Alisema
kuwa nivema ukaanzishwa utaratibu wa kuwapima wanafunzi ujauzito kila baada
ya miezi mitatu kwani hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza
mimba za utotoni ambazo zimekua zikisababisha wanafunzi wengi kukatisha masomo.
Mmoja
wa wanafunzi anayesoma katika shule ya sekondari Matai,(jina limehifadhiwa)
aliunga mkono ombi hilo,alisema kuwa iwapo mpango huo ukianza wanafunzi wengi
wa kike wataacha kufanya ngono kwani wataingiwa na hofu .
Kwaupande
wake katibu tawala wa wilaya hiyo, Frank Sichalwe aliwaonya baadhi ya wazazi
ambao wamekuwa wakishindwa kutoa ushirikiano pindi Watoto wao ambao ni
wanafunzi wanapopata ujauzito .
Alisema
kuwa kitendo hicho ni kinyume na sheria hivyo watambue kuwa huenda wakajikuta
wanafikishwa mahakamani lengo ni kuhakikisha kuwa wilaya hiyo inafanikiwa katika
kukabiliana na mimba kwa wanafunzi.
Comments
Post a Comment