Waziri
wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amewataka
wathibiti ubora wa elimu nchini kufanya kazi kwa weledi kwakuwa serikali
inathamini kazi zao na kuwategemea ili kuwa jicho la serikali katika kuonyesha
mahala penye mapungufu ili serikali iweze kuyafanyia kazi mapungufu hayo.
Prof.
Ndalichako amesema kuwa wakati mwIngine huwa inaumiza kuona vyombo vya habari
ndivyo vinavyoibua mapungufu yaliyopo mashuleni wakati wathibiti hao wakiwepo
na wakiwa wamekaa kimya na hivyo kuwataka kutokaa kimya pindi wanapoona kasoro
zilizomo mashuleni.
“Inauma
sana unapoona mambo ya elimu unayasoma kwenye vyombo vya habari, unakuta sijui
shule hii haina choo, shule hii sijui inachangamoto Fulani unajiuliza wathibiti
ubora wa eneo husika wako wapi, kwanini haya mambo hawayaoni ili tunapokuwa
tunapanga bajeti zetu tuwe tunaelekeza ‘resource’ zetu pale ambapo pana
uhitaji mkubwa, kwahiyo naomba sana wathibiti ubora tufanye kazi kwa ubunifu,”
Alisema.
Aidha
aliwataka wathibiti hao kuacha kufanya kazi kwa mazoea na kuwa kila jambo
linalohusu elimu linawahusu na kuwataka kutosita kutoa taarifa endapo kuna
jambo lolote kwani dhamira ya serikali ya awamu ya tano ni kutoa elimu bila ya
malipo lakini ni elimu iliyo bora kwani watoto wanapokwenda shule wakitoka wawe
wamesheheni ujuzi na maarifa ili waweze kutoa mchango chanya kwa
maendeleo ya nchi.
Prof.
Ndalichako aliyasema hayo kabla ya kuzindua ofisi ya wathibiti ubora wa shule
katika Wilaya ya Sumbawanga na Kalambo ,majengo
jengo ambayo yamejengwa kwa thamani ya shilingi billion 15.2 kwaajili ya ujenzi
wa ofisi hizo 100 nchini.
Comments
Post a Comment