Na. Faustine Pius Ng'habi
Kalambo.
Mlipuko wa furaha, vicheko na ndelemo umeliteka eneo la mwambao wa ziwa Tanganyika
kwenye ukanda unaomilikiwa na Wilaya ya Kalambo. Hii ni kufuatia tukio la
Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Kalambo Msongela Palela kufanya kikao na wavuvi, wakiwemo wafanyabiashara wa samaki na kuazimia kuanza
kutumika kwa soko la samaki la Kasanga mara moja kuanzia sasa ili lilete tija
kwa wananchi na Halmashauri kwa ujumla.
Soko la samaki la Kasanga ni moja kati ya masoko mawili likiwemo
soko la kimataifa la mazao lililoko Matai, masoko yaliyojengwa kuanzia mwaka
2009 hadi 2011 kupitia MVIWATA [Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania], ujenzi
wake ukifadhiliwa na jumuia ya Ulaya kwa asilimia 80 na asilimia 20 ya ujenzi huo ikitolewa na
Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kabla
Wilaya ya Kalambo haijamegwa na kuunda Halmashauri kamili ya Wilaya. Lengo
kuu la mradi huu, ni kuwaunganisha Wakulima ili wawe na sauti moja katika
kushawishi na kutetea maslahi yao kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kisiasa.
Soko hili liko umbali wa kilomita 73 kutoka Mji wa Matai
ambao ndio makao makuu ya Wilaya ukilenga kuwanufaisha takribani watu 35,205 wa
ukanda wa Ziwa Tanganyika na watu 238,000 kutoka maeneo mengine ya Wilaya ya
Kalambo. ]o-Hali kadhalika, mikoa kama vile Mbeya,Iringa, Njombe na Ruvuma
pamoja na nchi jirani za Zambia, Kongo D.R.C, Rwanda na Burundi ni fursa za Masoko
ya samaki zinazo vuliwa kutoka Ziwa Tanganyika na kuuzwa kupitia soko la samaki
la Kasanga.
Comments
Post a Comment