Serikali Yatoa Tahathari Ya
Ugonjwa Wa Ebola.
WANANCHI kutoka wilaya za Kalambo na Nkasi mkoani
Rukwa wameiomba serikali kuongeza vifaa vya
kupimia ugonjwa wa ebola pamoja
na kutolewa elimu kutokana na wilaya hizo kuwa na mwingiliano mkubwa wa watu kutoka
nchi jirani ya Congo na hivyo kuwa na hofu ya kuenezwa ugonjwa huo.
Wakiongea
katika nyakati tofauti wananchi hao,walisema serikali haina budi kudhibiti wahamiaji haramu kutoka nchi jirani
ya Congo kutokana na ugonjwa huo kuripotiwa kuwepo nchini humo.
Wakiwa
katika mkutano maalumu uliowajumuisha wataalamu wafya ngazi ya jamii na wadau
mbalimbali katika wilaya za Nkasi na Kalambo wamedai kuwa mazingira ya ugonjwa
huo ni hatarishi sana na hivyo vifaa vya kupimia ugonjwa huo vinatakiwa kwa
wingi hasa kutokana na mwingiliano mkubwa uliopo kati ya Watanzania na Congo.
Lakini
pia wizara ya afya imeshauliwa kuwatumia vyema Waganga wa jadi katika vita hii
ya ugonjwa wa ebola kwani watu hao wakielimika vya kutosha watatoa msaada
mkubwa kwa kuwaelekeza wateja wao kwenda hospitalini pale wanapobaini kuwa
wateja wao wanaonesha dalili ya ugonjwa huo
Awali
akitoa elimu kwa wananchi kutoka wilaya za Kalambo na Nkasi mwakilishi kutoka wizara ya afya Ashole Mshana
,alisema serikali imeanza kutoa tahadhari kwa wananchi dhidi ya ugonjwa huo na kuwasihi
wananchi hususani wanaoishi katika mwambao wa ziwa Tanganyika kuwa makini na
wageni wanaoingia kwenye maeneo yao
husika .
Mkuu
wa wilaya ya kalambo mkoani humo Julieth Binyura alisema lengo la serikali ni kuhakikisha ugonjwa huo hauingii nchini.
Aidha
aliwasihi wataalamu
kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya
athari za ugonjwa huo ikiwa ni pamoja
na kuongeza vifaa vya kupimia ugonjwa huo haswa kwa
wananchi wanaoingia kinyemera nchini kupitia njia za panya.
Comments
Post a Comment