SERIKALI imeanzisha kampeni maalumu ya kupambana na magonjwa
ya mifugo kwa kusambaza dawa katika majosho yote ikiwa ni jitihada
za kuwasaidia wafugaji ili kuondokana na changamoto ya kufa kwa mifugo
yao.
Ofisa mifugo mfawawidhi wa
kituo cha uchunguzi wa magonjwa ya mifugo kanda ya kusini
magharibi Dkt Kaini Kamwela,alisema kuwa huo ni mkakati wa serikali
katika kuhakikisha wafugaji wanafuga mifugo yao kitaalamu na
kuondokana na adha ya kufa kwa mifugo yao.
Alisema kwa muda mrefu
wafugaji wamekuwa wakikutana na chanagamoto ya kushindwa
kuongesha mifugo kutokana na ukosefu wa dawa pamoja na
gharama ya kuongeshea mifugo kuwa kubwa.
Alisema kwa kutambua
hilo serikali imepunguza gharama za kuongeshea mifugo
kwa asilimia mia moja.
Aliyasema hayo
mara baada ya kutembelea josho la kuogeshea mifugo lililopo
katika kijiji cha Kate wilayani Nkasi mkoani Rukwa.
Baadhi ya wafugaji katika
kijiji hicho waliipongeza serikali kwa jitihada hizo na
kusema kuwa awali
walikuwa wakiogesha mifugo kwa bei kubwa na hivyo
kusababisha kushindwa kumudu gharama sambamba na matibabu
kuwa bei juu.
"tunaishukuru sana
serikali kwa jitihada zake katika kuwapatia dawa za
mifugo pamoja na kuongeza idadi ya mashojo kwani hatua
hiyo itawawezesha kuondokana na changamoto ya kufa kwa mifugo
yetu’’ walisema wafugaji hao.
Comments
Post a Comment