Serikali Yafunga Machinjio Ya Nyama Katika Manisipaa Ya Sumbawanga

Eneo  la machinjio  ya nyama



Na Baraka lusajo.   Rukwa.

WAKAZI wa manispaa ya  Sumbawanga mkoani Rukwa wamelalamikia kufungwa ghafla kwa muda usiojulikana machinjio ya mifugo ya Manispaa hiyo kitendo kitakacho sababisha kukosekana kwa kitoweo cha nyama katika mji huo.
ENEO  LA MACHINJIO
Wakizungumza kwa nyakati  tofauti  wamesema kuwa machinjio hayo ndiyo  yanayotegemewa na wakazi wa Manispaa hiyo kwa na kufungwa bila kuwa na eneo mbadala kunaweza kusababisha kukosekana kabisa  kwa  kitoweo cha nyama, hivyo kuiomba serikali  kuteua eneo mbadala ili kuwawezesha wakazi hao  kuendelea kupata kitoweo  kama ilivyo kuwa hapo awali.
Alex mwita ni mmoja wa mkazi wa mji wa Sumbawanga, alisema kuwa serikali  haina budi kuweka utaratibu  maalumu utakao wawezeaha wao  kupata  kitoweo hicho  kwani walikuwa wamezoea  kwenda kununua  nyama kwenya  machinjio  hayo  lakini  kufungwa kwake  kutafanya   kukosa mboga ya kutumia  majumbani.
"Machinjio imefungwa ghafla  sana,nafikiri  kwamaoni yangu  serikali  ingetafuta njia mbadala ya kutunusuru na  suala  hili  kwani  hatuelewi  tutapata  wapi  tena  kitoweo cha nyama kutokana na  kuwa awali  tulikuwa  tukitegemea  hapa’’ alisema.
KATIKA PICHA NI KAIMU MSAJILI  WA BODI  YA NYAMA NCHINI
Awali akiongea  na wachinjaji  mifugo pamoja na wananchi,  Kaimu msajili wa bodi ya  nyama nchini,Imani Sichwale, amesema kuwa kalo hiyo ya mifugo haina vigezo vya  kuhifadhia nyama  na kusema kuanzia sasa  inafungwa rasmi.
‘’kalo  hii haina vigezo  na kibaya zaidi  imejengwa  katikati  ya  mji  hivyo  kuanzia leo imefungwa  na mkurugezi atawatafutia njia mbadala.’’alisema
Alisema kwa  kawaida  nyama haitakiwi  kugusa  chini wala  kuchinja  mifugo  ikiwa chini  kwani  kwa  kufanya  hivyo  kunafanya  walaji  wa  nyama kula nyama chafu.
Alisema kuwa Manispaa  kutumia kalo kama machinjio ni kosa na kusema kuwa suala  hilo atalipeleka kwa  mkurugezi  ili awatafutie wachinjaji sehemu mbadala ya kuchinjia mifugo yao.


Comments