Rc Wangabo Atoa Siku 30 Wakuu Wa Wilaya Kuanzisha Klabu Za Wapinga Rushwa

Katika picha ni  baadhi ya  maafisa  elimu  pamoja  na  walimu.

Mkuu wa mkoa wa Rukwa ,Joachim Wangabo ametoa mwezi mmoja kwa wakuu wa wilaya wa mkoa huo wahakikishe shule zote za msingi na sekondari zinaanzisha klabu za wapinga Rushwa lengo ni kuwawezesha wanafunzi kuwa wadilifu na viongozi bora wa badaye.

Akiongea kwa niaba ya mkuu wa mkoa huo, mkuu wa wilaya ya Sumbawanga Dkt, Halfan Haule wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kukabiliana na rushwa walimu wa shule  za msingi na sekondari pamoja na maafisa elimu mkoani humo,alisema lengo la serikali ni kutokomeza kabisa vitendo vya rushwa.
mwakilishi  wa  mkuu  wa mkoa  wa Rukwa

"kupitia hadhara hii ningependa kutoa wito kwa wakuu wa wilaya zote katika mkoa kuhakikisha kila shule ya sekondari na msingi katika wilaya husika inakuwa na klabu ya wapinga Rushwa na taarifa ya utekelezaji  niipate kabla au ifikapo mwishoni mwa mwezi februari" alisema.
katika  picha ni maafisa  elimu
Alisema kuwa katibu tawala wa mkoa ahakikishe maelekezo haya yanawafikia wakuu wa  wilaya kwa barua rasmi na nakala ya barua niione kwenye jalada. 
Alisema ili watoto na vijana wawe viongozi bora na wadilifu ,ni  lazima malezi yaanzie ngazi ya familia na kuendelezwa shuleni hasa shule za awali , msingi  na sekondari.
Mkuu wa  TAKUKURU mkoni humo,Hamza Mwenda, alisema Rushwa ni uozo wa kimaadili.
"maadili ni siraha muhimu katika mapambano dhidi ya rushwa kutokana na ukweli kwamba rushwa ni uozo wa kimaadili na maadili kwa maana ya mwenendo mwema hujengwa ndani ya mtu tangu anapozaliwa alisema Mwenda.
Hata  hivyo  mafunzo  hayo yameshirikisha  walimu  walezi wa shule  za  msingi na sekondari pamoja na maafisa  elimu katika shule zote  za  

Comments