Naibu Katibu Mkuu Atoa Siku Saba Ujenzi Kituo Cha Afya Samazi Kuanza Kujengwa.



  Na Baraka  Lusajo.
WAKAZI wa Kijiji cha Samazi wilayani Kalambo mkoani Rukwa wamelalamikia kucheleweshwa  kwa ujenzi  wa  kituo  cha  afya  ambacho   kilitakiwa  kujengwa  tangia june 2019 kutokana na  fedha  kutolewa na  serikali  kiasi cha shilingi  million  400 na hivyo  kuwa  na hofu  ya  fedha  hizo  kuhamishwa.

Malalamiko hayo waliyatoa mbele ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Dorothy Gwajima alipofanya ziara ya kikazi wilayani humo na kutembelea eneo linalojengwa kituo hicho cha afya.

Mmoja wa wakazi wa Kijiji hicho Saimon Kapesa alisema kuwa kutokana na kukosekana kwa kituo cha afya katika kata yao,wanalazimika kutembea umbali wa zaidi ya kilometa 20 kutafuta huduma za afya katika kata nyingine hivyo waliiomba serikali iwajengee kutuo hicho cha afya haraka ili kuwaondolea usumbufu.

"Katika Kijiji chetu, tunalazimika kutembea umbali wa zaidi ya kilometa 20 kutafuta huduma za afya, na hii ni tabu zaidi kwa akina mama wajawazito na watoto ambapo wakati mwingine wanahitaji huduma za dharura na pengine hata baadhi ya vifo vinavyotokea kijijini hapa vinatokana na kukosekana kwa matibabu kwa wakati" alisema.

Naye Monica Nakazwe mkazi wa Kijiji hicho alisema kuwa haoni sababu kwanini kuna kusua sua katika ujenzi wa kituo hicho ilihali serikali imekwisha toa fedha kwaajili ya ujenzi wa kituo hicho kwani kwa kufanya hivyo kunawasababishia usumbufu na gharama zisizokuwa za lazima katika kufuata huduma za afya katika vituo vya afya vya Ngorotwa na Matai, ambavyo vipo mbali na kijiji chao.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo, Nicholaus Mlango alisema kuwa ni kweli serikali imetoa fedha kiasi cha shilingi milioni 400 na tayari halmashauri hiyo imekwisha anza ujenzi wa kituo hicho cha afya.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Kalambo, Frank Sichalwe aliishukuru serikali  kwa kutoa fedha hizo ambapo tayari ujenzi wa kituo cha afya umekwisha anza na utakapo kamikika utaondoa kero zinazo wakabili wakazi wa kijiji hicho.

Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI, Gwajima alitishia kuzichukua fedha hizo kiasi cha shilingi milioni 400 zilizotolewa na serikali kwaajili ya ujenzi wa kituo cha afya cha samazi, huku akimpa siku saba Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmashauri ya Kalambo kuanza mara moja ujenzi wa kituo hicho ambacho umeshindwa kuanza kwa takribani miezi minane kutokana na mvutano wa eneo la ujenzi.



Comments