Kaya 47 Zabaki Bila Makazi Mkoani Rukwa.

KATIKA NI BAADHI  YA  WANANCHI  WALIOKOSA  MAKAZI

KAYA 47 zimebaki bila makazi baada ya nyumba 13 kubomoka kutokana na mvua kubwa iliyonyesha juzi katika kijiji cha kasitu kata ya sopa wilayani kalambo mkoani Rukwa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baada ya tukio  hilo kutokea ,wakazi wa kijiji hicho walisema kuwa mvua hiyo ilikuwa kubwa na imeambatana na upepo mkali ilianza kunyesha majira ya saa nane na  dakika  arobaini  na tano mchana na kusababisha kubomoka nyumba  hizo.
Anold Yolam,mkazi wa  kijiji  hicho  alisema kuwa baadhi ya watu ambao nyumba zao zimebomoka  wamepewa hifadhi kwa  mwenyekiti  wa serikali  ya  kijiji na wengine  wamepewa hifadhi kwa majirani na kuiomba  serikali iwasaidie.
Naye Jeriko Malema alisema kuwa mvua hiyo ilinyesha kwa  muda  mfupi lakini iliambatana na upepo mkali  na hali itasababisha  kubomoka kwa nyumba hizo.

Kwaupande wake ofisa mtendaji wa kijiji hicho Gasper Kateka alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa nyumba 13 zimeanguka na kuwaacha watu 47 bila makazi.
Alisema kuwa baadhi ya wananchi ambao nyumba zao zimebomoka wamepewa hifadhi kwa  mwenyekiti wa kijiji  na wengine  kwa  majirani  wakati  wakisubiri  msaada zaidi.
Mwenyekiti  wa  kijiji  hicho John Sizo  alisema kuwa wananchi wengine ambao hawakupatwa na janga hilo wanawajibu wa kuwasaidia watu waliopatwa na maafa hayo.
Mkuu wa wilaya ya Kalambo Julieth  Binyura,  alisema tukio hilo limetokana  na wananchi kutojenga nyumba imara  na zenye  ubora kwani ndizo zitakazo saidia kuondokana na adha  hiyo.
Alisema nyumba nyingi zilizo athirika hazikuwa zimejengwa kwa kufuata taratibu za ujenzi bora hivyo wananchi wanapaswa kuwashirikisha wataamu wa  halmashauri pindi wanapo jenga  nyumba  zao ili wawape ushauri wa namna ya kujenga nyumba bora.

Comments