Wananchi waipongeza Serikali kwa kusambaza Madaktari Bingwa

kushoto  ni mkuu  wa  wilaya  ya  Kalambo akiungana na wananchi katika  kupima afya katika kituo  cha afya Matai 


 Na  Baraka Lusajo.Kalambo.
Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa imeanzisha utaratibu maalum wa kuwasaidia wananchi kwa kusambaza Madaktari Bingwa katika vituo mbalimbali vya afya lengo ikiwa ni kuondokana na changamoto ya kutembea umbali  mrefu kwaajili ya kutafuta matibabu.
katika  picha ni mkuu  wa  wilaya  akipima afya  na mganga  mkuu  wa  wilaya  hiyo Aleni  Mlekwa ikiwa ni jitihada  za kuhamasisha  wananchi  kujitokeza kujua  afya  zao.
Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo Aleni Mlekwa alisema kuwa madaktari hao wamesambazwa katika vituo vyote vya afya wilayani  humo ambavyo ni kituo cha afya cha Mwimbi, Matai na Ngorotwa.
Alisema kuwa lengo ni kuwezesha wananchi kuondokana na adha ya kutembea umbali  mrefu kwaajili ya kufuata huduma za matibabu.
Madaktari hao walichukuliwa kutoka hospitali ya mkoa wa Rukwa na wananchi elfu mbili wamekwishatibiwa na zoezi hilo bado linaendelea.
Alisema kutokana na mwitikio wa watu kuwa mzuri wameongea na uongozi wa  Wilaya ili  katika  awamu ijayo  bajeti iongozwe kwa lengo  la kufikisha huduma hiyo  katika  zahanati zote za wilaya hiyo.
"Katika zoezi hili tuna madaktari wa aina mbalimbali ikiwemo wa Macho,  Madaktari  wa magonjwa  ya ndani, madaktari wa magonjwa  ya akina mama, Madaktari wa magonjwa ya watoto pamoja na Madaktari  wa upasuaji na   tunaishukuru  sana  serikali  kwa  kutoa   fedha  ili  kuwasaidia  wananchi  wanaoishi  katika  maeneo  ambayo hayafikiki kiurahisi,"Alisema  Mlekwa.
Mmoja wa Madaktari bingwa mkoni humo,Hamisi Ulaya alisema  mwitikio wa wananchi umekuwa mzuri  kwani kila sehemu waliyopita  watu walikuwa na uhitaji wa kutibiwa.
Mkuu wa wilaya ya Kalambo Bi. Julieth Binyura, aliwasihi wananchi  wilayani  humo kuendelea  kujitokeza kwa wingi  kwenye  zoezi  hilo ili kupata  matibabu katika maeneo hayo.
Alisema lengo la Serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha  wananchi  wanaondokana  na adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta huduma za matibabu na kuwataka wahudumU wa  afya  kutoa  vitambulisho  kwa  wazee  wote.
katika  picha  ni baadhi  ya  wananchi  waliojitokeza kipima afya zao katika  kituo cha afya cha Mwimbi.
Baadhi ya wananchi wilayani humo wameipongeza Serikali kwa kusogeza huduma  za matibabu  karibu  na maeneo  yao na kuomba  kuwa na utaratibu  maalumu  wa  kurudiwa  kwa  zoezi  hilo. 

Comments