Rc Wangabo Azindua Shamba la Mkulima Wilayani Kalambo. Awataka Wananchi Kulima Kilimo Chenye Tija.




KATIKA  PICHA   KULIA  NI MKUU  WA  MKOA  AKIWA ANAWALEKEZA WAKULIMA 

 Na  Baraka  Lusajo. Kalambo.
Wakulima mkoani Rukwa wamelalamikia kukosekana kwa pembejeo pamoja na bei elekezi katika msimu huu wa kilimo hali inayotia hofu kutopata mavuno  makubwa kutokana na wakulima wengi kulima bila kutumia pembejeo na kuiomba  Serikali kuweka utaratubu maalumu wa kusambaza pembejeo kabla ya msimu  kuanza.
Wakiongea wakati wa uzinduzi wa baadhi ya mashamba katika  kijiji cha Kalalasi Wilayani Kalambo yaliozinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Joachim  Wangabo.

KATIKA PICHA NI MKUU  WA  WILAYA  YA  KALAMBO JULIETH  BINYURA AKIPANDA MBEGE ZA MAHINDI  KATIKA  SHAMBA  LA MKULIMA.

Walisema wamekuwa wakikabiliwa na changamotoya kucheleweshewa kwa   pembejeo za kilimo na kuwalazimu kutumia pembejeo ambazo si bora.
Walisema serikali haina budi kuweka utaratibu maalumu ambao utawawezesha  kupata  pembejeo mapema kabla ya msimu kuanza .
‘’Tunaiomba Serikali kuanzisha utaratibu mzuri ambao utatuwezesha kupata  pembejeo mapema kwani kila mwaka pembejeo hususani mbolea na mbegu  zimekuwa zikiletwa kwa kuchelewa sana.”
KATIKA PICHA    NI KATIBU  TAWALA  FRANK  SICHALWE AKILIMA   NA NYUMBA YAKE NI  MKURUGEZI  WA  HALMASHAURI YA KALAMBO MSONGOLA  PALELA .
Aidha, waliipongeza serikali mkoani humo kwa kuweka utaratibu wa  kuwatembelea mashambani na kuwa utaratibu huo utawasaidia kwa  kiasi  kikubwa  kuhamasika  na kulima kilimo bora na chenye tija.
Afisa kilimo Mkoani humo Ocran Chengula, alisema pembejeo za kilimo zipo za kutosha na kusema shida ni wakulima wengi  kuwa na mazoea ya kununua pembeo pindi  msimu  wa  kilimo  unapoanza.
‘’Pembejeo zipo za kutosha, tatizo ni kwamba  wakulima  wengi  wamezoea    kununua  pembejeo  wakati msimu unapoanza ilihali  kwenye  maduka na maghara  ya pembejeo katika misimu yote zinakuwa zipo, hivyo  wakulima  mjipange  mnaweza kununua pembejeo muda na wakati wote badala ya kusubiri  kuanza kwa  msimu, alisema Chengula.
  Awali akikagua mashamba ya wakulima Wilayani Kalambo, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Joachim Wangabo, aliwasihi wakulima kulima kilimo chenye  tija  na ambacho  kitawasaidia  kujikwamua  na hali  ya kiuchumi.
Alisema kila  mkulima  anawajibu  wa  kuwatumia  wataalamu  wa  kilimo kwenye maeneo husika ikiwa  ni pamoja na kutumia  mbolea  na viuatiulifu kwa lengo la  kupata mavuno mengi.
‘’Endapo tukifanya  hivyo tutaweza  kufikia  malengo  yetu  ya  kimkoa  ambapo  mwaka jana tulikuwa  na  tani laki nne na  tisini na nne  na mwaka  huu  tunataka  kufikia tani laki saba za mahindi  peke  yake, lakini tutaweza  kufikia  kiwango  hicho endapo tutalima kilimo chenye tija.” Alisema Wangabo.


Comments