Rc Wangabo Awataka Wananchi Kulima Kilimo Chenye Tija.

KULIA NI MKUU  WA  MKOA  WA  RUKWA AKIONGEA  NA  WAKULIMA KATIKA BONDE  LA ZIWA  RUKWA

Wakulima wa zao la alizeti katika bonde la ziwa Rukwa wilaya ya Sumbawanga  mkoani Rukwa wameiomba serikali  kuweka  bei elekelezi kwenye  mbegu ya zao hilo kutokana na gharama  kuwa juu  hivi  sasa hali inayosababisha baadhi yao kushindwa kulima zao hilo.

Wakiongea kwa nyakati  tofauti  wakati wa mandalizi ya zao  hilo kwenye mashamba yao ,wamesema kuwa changamoto  kubwa ni  ukosefu  wa masoko  na bei ya  mbegu  kuwa  kubwa kiasi kwamba wanahofu baadhi yao watashindwa hata kulima zao hilo katika msimu huu.
Wamesema serikali haina budi  kuweka  bei  elekezi  ya  mbegu   ya  zao  hilo  kama  ilivyo  kwa  pembeo nyingine  za kilimo kwa lengo la kuwasaidia kuinua kipato chao.
"tunaiomba serikali itutafutie  masoko ya uhakika kwani  kwa  huku kwetu bondeni kuzalisha tunazalisha  sana  alizeti lakini  tatizo ni wapi utaipeleka"walisema.

Afisa kilimo wilayani Sumbwanga Joseph Bakuli amesema lengo ni kuwa zao la alizeti kuwa miongoni mwa mazao ya  kimkakati ndani ya mkoa hivyo wananchi wanawajibu wa kulima zao hilo na kuondokana na kutegemea  zao moja la mahindi.

Naye mkuu wa mkoa wa Rukwa ,Joachim  Wangabo,  amewataka  wananchi  kufuata  kanuni  bora  za kilimo  kwa  kuwashirikisha wataamu  lengo likiwa  ni  kufikia  mafanikio.

Hata hivyo katika msimu wa kilimo wa mwaka 2018/2019 jumla ya hekta 66,872.15 za alizeti zililimwa katika mkoa  wa Rukwa na kupatikana tani 61,651.11.


Comments