katika picha kushoto ni mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangaboakitoa sadaka |
Na Baraka Lusajo. Rukwa.
Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amesisitiza umoja na
mshikamano kwa waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)ambao
kwa majuma kadhaa wamekuwa na mikwaruzano hali iliyofanya waumini hao kuswali
kwa mafungu jambo ambalo halileti maendeleo ndani ya kanisa pamoja na mkoa.
kulia ni mkuu wa mkoa akisalimiana na asikofu wa kanisa la kkkt |
Amesema kuwa wakati alipoteuliwa na Rais Dkt. John Pombe
Magufuli na kuweza kuwasili katika mkoa miongoni mwa viongozi wa dini
waliomuombea alikuwa ni Baba Askofu Ambele Mwaipopo ambaye anatambuliwa na
serikali na kutahadharisha kuwa endapo serikali inamtambua kuwa ndio kiongozi
wa kanisa hilo iweje wanaushirika wasimtambue.
“Mimi niko ndani ya Kanisa, nalitambua Kanisa, namtambua Muasham
Baba Askofu, Kanisa hili limesajiliwa, Kanisa la Mungu, Muasham Baba Askofu wakati
nilipofika tu hapa Mkoa wa Rukwa, Sumbawanga. Pamoja na viongozi wengine
waliofika ofisini wakaniombea, Baba Askofu huyu alikuja akaniombea pia, wewe ni
nani usiyemtambua? Mimi niwatake na kuwaomba, wanausharika wote ambao wako nje
ya Kanisa warudi ndani ya Kanisa,” Alisema.
katika picha ni mkuu wa mkoa wa Rukwa akiongea na waumini |
Na kuongeza kuwa endapo waumini wakishikana Mungu huwa pamoja na
waumini hao na kamwe Mungu hawezi kumfuata mtu asiyependa umoja na
kuwahahakikishia kuwa wale wote ambao wapo nje ya Kanisa kuwa Baba Askofu
amekwisha wasamehe hivyo wasiwe na sababu ya kuendelea kubaki nje ya Kanisa.
Ameyasema hayo aliposhiriki ibada ya ya katika kanisa la KKKT
Dayosisi ya Ziwa Tanganyika Mkoani Rukwa.
katika picha ni asikofu wa makanisa ya KKKT |
Kwa upande wake Baba Askofu Ambele Mwaipopo alimshukuru Mkuu wa
Mkoa huyo kwa kutoa ujumbe mzuri wa mshikamano na kuwaomba waumini
waliohusdhuria ibada hiyo kuzungumza na wale wote waliopo nje ya kanisa hilo
ili kuweza kuurudisha umoja na kuweza kupanga mambo ya kimaendeleo.
Comments
Post a Comment