Na Baraka Lusajo. Kalambo
MTOTO Maren
Namsukuma (7) amefariki dunia na watu wengine 30 wamepata matibabu katika zahanati ya Kalembe Kijiji cha Utengule
kata ya Mambwe Nkoswe wilayani Kalambo mkoani Rukwa baada ya kula mzoga wa
nguruwe.
Kwamujibu wa taarifa
ya kamanda wa polisi mkoani Rukwa Justine Masejo ilisema kuwa siku ya Desemba
21 Osward Simpungwe alichinja nguruwe ambaye alikuwa amekufua mwenyewe na kisha
kuanza kuuza nyama.
Wakazi wa kijiji hicho
akiwemo baba wa marehemu walinunua nyama hiyo na kuitumia kwaajili ya kitoweo,
ndipo waliokula nyama hiyo walianza kuugua ugonjwa ambao haukujulikana mara
moja.
Kabla ya kufariki
mtoto huyo familia nzima walilalamika kuumwa tumbo, ndipo baba yao alipokwenda
kwenye duka la dawa muhimu za binaadamu na kununua Flagyl pamoja na Panadol na
kumpatia mtoto huyo,lakini hata hivyo hazikumsaidia na hali yake ilizidi kuwa
mbaya na ilipofika majira ya saa 10 usiku siku ya Desemba 25, alifariki dunia
wakati wakienda katika zahanati ya Kijiji kupata matibabu.
Mmoja wa wakazi wakazi
wa Kijiji hicho aliyenusurika baada ya kula nyama hiyo, Aberi Sinyangwe
alisema kuwa katika Kijiji hicho kumekuwa na changamoto ya
kutokea matukio hayo kutokana na kukosekana kwa maafisa mifugo ambao
wanajukumu la kukagua ubora wa nyama kabla ya kuliwa na binaadamu.
Aliiomba
serikali kupeleka wataalamu hao kwa ili waondokane na tatizo
la kujirudia kwa matukio hayo.
Mwenyekiti wa kijiji
hicho Wigani Namsukuma alisema kuwa baada ya serikali ya kijiji kupata taarifa
za tukio hilo ilitoa taarifa polisi na kisha kuwakimbiza katika zahanati ya
Kijiji wagonjwa 30 waliougua baada ya kula nyama hiyo na walipatiwa matibabu
lakini kwa bahati mbaya alifariki mtoto huyo.
Naye ofisa mifugo
wa wilaya ya Kalambo, Enos Luvinga aliwaonya wakazi wa Kijiji hicho
kuacha tabia ya kula nyama za mifugo inayo jifia yenyewe kwani ni
hatari kwa afya zao kwakua mifugo hiyo inakuwa na magonjwa ndiyo maana inajifia
yenyewe.
Kaimu Mganga mkuu was
wilaya ya Kalambo Rock Sabuni aliwashauri wakazi wa kijiji hicho kuacha tabia
ya kujinunulia dawa na kutumia bila kupata ushauri wa daktari, badala yake
wanapougua wawe wanakwenda haraka katika zahanati na vituo vya afya kwaajili ya
matibabu.
Kamanda Masejo alisema
kuwa Simpungwe anashikiliwa na polisi kwa mahojiano kutokana na kosa la
kuwauzia watu nyama ya mzoga huo na atafikishwa mahakamani baada ya mahojiano
hayo kukamilika.
ReplyDeleteNi hatari sana kula mizoga iliyojifia. Mabadiliko yanahitajika, na yanaanzia kwako wewe mwananchi!. Chukua hatua, okoa maisha yako na ya jamii yako!