Mlima wa changamoto unaomkabili Freeman Mbowe kuelekea 2020

Ni matokeo yaliyotarajiwa, Freeman Mbowe ambaye amekiongoza chama kikuu cha upinzani Tanzania Chadema kwa miaka 15, amepewa tena ridahaa na wanachama kushikilia usukani wa chama kwa miaka mitano ijayo.Mbowe na Zitto
Upinzani dhidi yake kwa mwaka huu, kama ilivyokuwa miaka mitano iliyopita ulikuwa ni hafifu, akishinda uchaguzi huo uliofanyika Jumatano wiki hii alishinda kwa kishindo cha asilimia 93.5.
Baada ya kutangazwa mshindi, wafuasi wake kwa furaha wakamuimbia: "...tuvushe mwamba tuvushe."
Mwamba anayezungumziwa ni Mbowe, lakini awavushe kutoka wapi na kuelekea wapi ni jambo ambalo kila mtu anaweza kuwa na tafsiri yake.
Moja ya tafsiri inaweza kuwa kuwavusha kutoka kwenye changamoto zinazowakumba kwa sasa, na katika hilo changamoto ni za upinzani kwa ujumla.
Chadema ikiwa kama chama kikuu cha upinzani kiongozi wake anatazamwa pia kuwa kama kiongozi mkuu wa upinzani kwa ujumla wake.Awamu hii ya nne madarakani kwa Mbowe inaanza zikiwa zimesalia wiki mbili tu uingie mwaka 2020,Haki miliki y

Comments