Mto Kalambo |
Na Baraka Lusajo. Kalambo.
Kivuko cha mto Kalambo |
MWANAMKE
mjazito aliyefahamika kwa jina la Maria Kalunde miaka(42) pamoja na mtoto
wake Magreth Lui(9) wamekufa maji baada ya kutumbukia katika mto Kalambo
kutokana na kuteleza katika kivuko cha miguu cha mto huo.
Tukio
hilo limetokea juzi katika kijiji cha kasitu kata ya Sopa wilayani Kalambo
mkoani Rukwa wakati watu hao wakivuka katika mto huo
Akizungumzia
tukio hilo mmoja wa wakazi wa kijiji hicho, Nobert Mwanawima alisema mwanamke
huyo mjamzito pamoja na mtoto wake walikufa maji kutokana na eneo hilo kutokuwa
na daraja la kuvukia kitendo kilichosababisha wananchi wa kijiji hicho
kutengeneza kivuko cha miguu kinachokatisha mto kwa kutumia miti.
Alisema
kuwa mwanamke huyo alipokuwa akipita katika kivuko hicho pamoja na mwanaye
waliteleza na kuangukia mtoni, na kisha walianza kupiga kelele
za kuomba msaada, lakini kwakuwa watu walikuwa mbali hawakufanikiwa
kufika kwa wakati kuwasaidia.
''siku moja baadaye walipata taarifa kuwa miili yao
ilipatikana katika kijiji jirani na wakazi wa kijiji hicho waliamua
kufanya maziko, ndipo walipoamua kuchukua msiba na kuusafirisha hadi
kijiji cha Katete walipokuwa wakiishi mama huyo pamoja na mwanaye''
alisema.
Naye Jelemia shigoma
mkazi wa kijiji cha Kasitu , alisema kuwa kutokana
na changamoto ya kutokuwa na daraja katika eneo hilo watu wamekuwa
wakifa maji kutokana na kusombwa na maji hali hiyo imekuwa
ikijitokeza mara kwa mara katika nyakati za masika kwakuwa mto huo unakuwa
umejaa maji.
Aliiomba serikali kuwajengea daraja
katika eneo hilo ili kuepukana na vifo vinavyotokea mara kwa mara kwani wao
wamekuwa hawajisikii vizuri kushuhudia watu wakipoteza maisha kila nyakati za
masika.
Ofisa
mtendaji wa kijiji hicho Gasper kateka ,amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na
kuongeza kuwa hapo awali hali ilikuwa mbaya zaidi kwakua hakukua hata hicho
kivuko lakini kilipatikana baada yawananchi kujichangisha
fedha kiasi cha shilingi 10,000 kila mmoja kwaajili ya
kuwalipa mafundi waliokitengeneza.
Diwani wa kata hiyo Richad Kamagari
,alisema tatizo la vifo kutokana na kutumbukia watu mtoni limekuwa likijitokeza
mara nyingi na yeye amekwisha toa taarifa katika baraza la madiwani la
halmashauri ya wilaya ya Kalambo.
Kwaupande wake kaimu katibu tawala
wa wilaya ya Klambo,Mahmood Shauri amethibitisha kutokea kwa tukio hilo
na kusema kuwa serikali itajitahidi kutatua changamoto hiyo inayowakumba wakazi
wa kijiji hicho.
Comments
Post a Comment