Katibu Mkuu Atoa Siku 90 Kituo Cha Afya Samazi Kujengwa




KATIBUmkuu ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa(Tamisemi),Joseph Nyamuhanga ametoa siku 90 kwa halmashauri ya wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa kuhakikisha inaanza ujenzi wa kituo cha afya Samazi vinginevyo itanyang'anywa fedha zilizotolewa kwaajili ya ujenzi wa kituo hicho.

Agizo hilo alilitoa hivi karibuni alipokuwa katika ziara ya kukagua maendeleo ya ujezi wa vituo vya afya  pamoja na  hospitari za wilaya katika mkoa wa  Rukwa.

Alisema kuwa serikali ilitoa  fedha muda mrefu, kiasi  cha  shilingi  milioni 400 kwaajili ya ujezi wa kituo hicho cha afya lakini mpaka sasa ujezi wake haujaanza kitendo ambacho ni kuchelewesha huduma kwa wananchi.

"Serikali imetoa maelekezo na sio muanze tena marumbano ya wapi kijengwe kituo hicho kama mtaendelea na hali hii mtanyang'anywa fedha hizo wapewe wengine wanao zihitaji na wako tayari kutekeleza maelekezo ya serikali kwa wakati" alisema

Aidha aliekeza kuwa kwakuwa katika Kijiji hicho tayari kuna  zahanati ,nibora iliopo ipanuliwe ili kuwe na majengo mengi ambayo yatakidhi mahitaji ya sasa ambapo ilichopo imeonekana ni ndogo kutokana na idadi ya watu waliopo wakati huu.

Aidha alisema kuwa serikali  inategemea kutoa fedha kiasi  cha shilingi milioni 300 kwa  kila hospitali ya wilaya kwa ajili ya kukamilisha ujenzi na aliwaagiza wakurugezi nchi nzima  kuzitumia fedha  hizo vizuri ili zikidhi mahitaji.

Hata hivyo imeelezwa  kuwa zaidi ya vituo vya afya 350  vipya vimejengwa nchi nzima na vituo vingine 67 vinatarajiwa kujengwa ifika  mwaka  2020.



Comments