HALMASHAURI ya wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa
inakabiliwa na upungufu wa watumishi 2,693 hali inayochangia wananchi kutopata
huduma wanazotaka kwa muda muafaka.
Hayo yalibainishwa hivi karibuni na afisa
mipango wa halmashauri hiyo,Eric Kayombo wakati akiwasilisha bajeti ya shilingi
bilioni 36.4 kwanye baraza la madiwani wa halmashauri hiyo ambayo iliipitishwa
na baraza hilo na itakuwa bajeti ya mwaka wa fedha 2020/2021.
Alisema kuwa halmsahauri hiyo inauoungufu
mkubwa wa watumishi kitendo kinachosababisha baadhi ya huduma wanazohitaji
wananchi kutozipata kwa wakati kutokana na upungufu huo.
Ofisa mipango huyo wa halmashauri hiyo alisema
kuwa hali hiyo imetokana na baadhi ya watumishi kuondolewa kazini kutokanana na
kuwa na vyeti bandia hivyo kupoteza sifa za kuwa watumishi wa umma.
Akiwasilisha bajeti hiyo, Kayombo alisema
halmashauri hiyo katika mwaka wa fedha wa 2020/2021 inategemea kutumia shilingi
bilioni 27.0 kwaajili ya kulipa mishahara,shiringi bilioni 5.6 kwaajili ya
miradi ya maendeleo, bilioni 1.8 kwaajili ya matumizi mengineyo.
"kwa upande wa makusanyo ya ndani
halmashauri hiyo inatarajia kukusanya shilingi bilioni 1.8 kutokana na vyanzo
vyake mbali mbali" alisema ofisa mipango huyo.
Baraza hilo liliipitisha bajeti hiyo kwa
asilimia mia moja huku mwnyekiti wake Daudi Sichone akiwaasa wananchi kuona
umuhimu wa kulipa Kodi na tozo mbalimbali ambazo zitawezesha kutekeleza miradi
ya maendeleo.
Comments
Post a Comment