Halmashauri Ya Kalambo Yaanzisha Kampeni Ya Upandaji Miti Ya Vivuli Na Matunda.

Kushoto  ni  mkurugezi mtendaji Palela Msongela wakiwa mapumziko na katika tawala Frank Sichalwe baada  ya  kutoka kwenye shughuli ya upandaji miti.


KATIKA jitihada za kutunza na kuhifadhi  Mazingira, Halmashauri ya wilaya ya  Kalambo mkoani Rukwa imeanza utaratibu maalumu wa kupanda miti katika maeneo  tofauti ya wilaya hiyo na tayari imefanikiwa  kupanda miti 1200 katika mji wa Matai.
Mmoja  wa  watumishi akipanda miti katika  eneo  la halmashauri.
Kaimu afisa mazingira wilayani humo Majanael Swalehe, alisema zoezi hilo litakuwa endelevu,ambapo wanatarajia kila jumamosi ya mwisho wa mwezi watakuwa wanapanda miti katika maeneo  mbalimbali ya Halmashauri hiyo ikiwa  ni jitihada za kusaidia kutunza na kulinda mazingira ili yasiharibike.
"mpaka sasa tumefanikiwa kupanda miti 1200 na ili kuendeleza jitihada hizo tumeamua kuwa kila jumamosi  ya mwisho wa mwezi tutakua tunaendelea na  kampeni hii na mwisho wa mwezi huu tutapanda miti  katika eneo la  hospitali  ya  wilaya" alisema ,Mjanaeli .
Mkurugezi  mtendaji  wilayani  kalambo Msongela Palela akipanda miti
Hata hivyo siku ya Desember  8 ambayo ilikuwa siku ya kumbukumbu ya  uhuru   wa Tanganyika,wilaya ya  kalambo  ilitumia  siku   hiyo kupanda miti  kuzunguka   maeneo  yote  ya  ofisi za Halmashauri ambapo  viongozi  mbali mbali  wa  wilaya  walijitokeza  kushiriki zoezi hilo.

Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Msongela  Palela aliwataka wananchi kuwa  na utaratibu wa kupanda miti katika  maeneo  yao  ikiwa  ni  jitihada  za kuzia upepo  ili  usiharibu  makazi yao na huku  katibu  tawala  wilaya hiyo, Frank Sichalwe aliwapongeza wananchi  kwa  kujitokeza kwa wingi katika zoezi  hilo.

‘’tunawapongeza wananchi  kwa kujitokeza kwenu lakini ni vizuri mkawa na utaratibu wa kupanda miti katika  maeneo ya makazi yenu ili kuhifadhi  na kutunza mazingira.’’walisemaa viongozi  hao.


Comments