Na Baraka Lusajo. Kalambo.
HALMASHAURI
ya wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa imepitisha bajeti ya shilingi bilioni 36.4
katika mwaka wa bajeti 2020/2021.
Akisoma
bajeti hiyo jana katika baraza la madiwani lililofanyika katika ukumbi wa
mikutano wa chuo cha Makatekista uliopo mjini Matai, Afisa mipango wa
halmashauri hiyo Eric Kayombo ,alisema kuwa katika bajeti hiyo halmashauri
imepanga kukusanya mapato ya ndani shilingi bilioni 1.8.
Alisema
kuwa fedha bilioni 27.0 zitatumika kwaajili ya mishahara, shilingi bilioni 5.6
zitakuwa kwaajili ya miradi ya maendeleo na shilingi bilioni 1.8 ni kwaajili ya
matumizi mengineyo.
Katika
kikao hicho mwenyekiti wa halmashauri hiyo,Daudi Sichone aliwaomba madiwani wa
halmashauri hiyo kwa kushirikiana na wananchi wajitahidi kujenga vyumba vya
madarasa pamoja na maboma kwaajili ya zahanati na vituo vya afya kwakuwa hivi
sasa serikali inatoa hela kwaajili ya kumalizia.
Alisema
kuwa vijiji ambavyo havijishughulishi wao watakosa maendeleo kwakua serikali
inatoa fedha kukamilisha maboma ambayo bado, hivyo ni lazima wananchi waanze
ndipo serikali imalizie.
Naye
mkuu wa wilaya ya Kalambo Julieth Binyura aliwataka wananchi wanaoishi vijiji
vilivyopo maeneo ya mpakani kuwa makini na wageni wanaoingia,wasiwapokee
kiholela badala yake watoe taarifa kwa vyombo vya ulinzi.
Alisema
kuwa katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka kuna sikuu hivyo watu wasio wema
wanaweza kutumia fursa hiyo kuingia nchini na kufanya uhalifu.
Comments
Post a Comment