HABARI ZA HIVI PUNDE. Baadhi Ya Wananchi Walazimika Kuyahama Makazi Yao Kutokana Na Maji Ya Mvua Kujaa Kwenye Kingo Za Nyumba Zao.
Baadhi
ya wananchi katika mji wa Kasanga wilayani Kalambo mkoani Rukwa wamelazimika
kuyahama makazi yao nyakati za usiku baada ya maji kujaa hadi kufikia usawa madirisha
kufuatia mvua kubwa ilionyesha
usiku wa kuamkia Desember 29,2019.
Kwa
mujibu wa afisa tarafa ya Kasanga Endrue Manyema Ngindo , amesema baadhi ya
nyumba za kulala wageni pamoja na nyumba za
wananchi ziliweza kujaa maji na
kupelekea kuyahama makazi yao.
‘’baadhi
ya nyumba za kulala wageni ikiwemo ya Atupenda ‘’A’’ inayomilikiwa na Rhoda Maseba
ilikuwa ndani ya maji usawa wa madirisha na kusabisha wateja wake kuhama usiku
huo’’alisema Ngindo.
Aidha
aliongeza kwa kusema nyumba ya Dorcas Nakazwe moja ya ukuta wa nyumba yake ulibomoka
na kupelekea wapangaji wake kukimbia usiku
huo .
Comments
Post a Comment