KABURI LA CHIFU |
WANANCHI wa kata ya
Mambwekenya Wilayani Kalambo wamejikuta katika sintofahamu baada ya kuzuiliwa
kushiriki mazishi ya kiongozi wa baraza la machifu mkoani Rukwa ,chifu
Christofa Kutazungwa aliyezikwa bila jeneza huku akiwa amekaa kwenye kiti chake
na ngozi ya ng’ombe ikilazwa chini badala kumzika mtu mzima kama
sadaka.
KAMATI YA KUCHIMBA NA KUFANYA MAZISHI YA CHIFU |
Wakiongea kwa nyakati
tofauti wakati mazishi ya chifu huyo wamesema mazishi ya machifu yamekuwa yakifanyika
nyakati za usiku tofauti na mazishi hayo ambayo yamefanyika mchana
na huku watu wakizuiliwa kulia na kushiriki kuchimba kaburi pamoja na
maziko.
MWILI WA CHIFU UKIPELEKWA MAKABURINI KWA AJILI YA MAZISHI NA HUKU UKIWA UZUNGWA NA AKINA MAMA |
John Sichula mkazi
Kijiji cha Mambwekenya ,alisema kwake tukio hilo
limekuwa la kwanza kuona mtu akizikwa bila jenaza
na kusema wamezoa kushiriki katika mazishi ikiwemo
kuchimba makaburi lakini imekuwa tofauti kabisa
na mazizishi ya chifu huyo.
Alisema licha ya
hilo wamezoea kuona mazishi ya machifu yakifanyika
nyakati za usiku lakini imekuwa tofauti kwa
kiongozi huyo kutokana na kuzikwa muda wa mchana huku
kila mtu akiwa anaona na hivyo kuonekana ni kitu
kigeni kwao.
Naye Boidi Sichula
mkazi wa maeneo hayo ,alisema kilicho mshangaza
ni kuona chifu anazikwa akiwa amekaa na ngozi ya
ng’ombe kutandikwa chini na kusema katika maisha yake
yote hajawahi kuona kitu kama hicho.
Daud Mbaya
makazi Wa maeneo hayo,alisema kilicho mshangaza
zaidi nikuona watu wakizuiliwa kushiriki mazishi
hayo pamoja na kulia wakati wa msiba.
‘’tumezoea akina
mama wakilia wakati wa msiba lakini imekuwa
tofauti kwa kiongozi huyo kutokana na watu kuzuiliwa
kulia zaidi ya kucheza ngoma na kuiomba nyimbo’’alisema .
kwa upande wake kiongozi
anaesimika machifu mkoani humo Richad Sinyangwe,alisema wanazika na ngozi ya
ng’ombe ikiwa ni badara ya sadaka ya kumtoa mtu.
Alisema kipindi
cha nyuma ilikuwa ni lazima kiongozi
mkubwa kama huyo kuzikwa na mtu aliye
hai lakini badae walikaa na kufanya maboresho na kuanza
kutumia ngozi ya mnyama pamoja na damu ya mnyama
kama ishara ya sadaka.
Alisema
kufanya hivyo kuna onyesha kuwa sadaka inapokelewa
na mizimu na kusema hakuna madhara yoyote yanayoweza kutokea
.
MACHIFU WALIO HUDHULIA KWENYE MSIBA HUO |
Kwa upande
wake chifu Ntono wa nne wa himaya ya Ulungu Maiko
Sikazwe ,alisema chifu huyo amezikwa na ngozi na akiwa amekaa
lengo ikiwa ni kudumumisha mila ya kichifu.
Mwakilishi wa mkuu
wa mkoa huo, Julieth Binyura ambayepia ni mkuu wa wilaya ya
Kalambo,alisemac hifu huyo ndie aliyekuwa kiongozi mkuu wa machifu mkoani
humo na kifo chake kimewachia simanzi kubwa kutokana na uadilifu
aliokuwa nao enzi za uhai wake.
Aidha aliwataka
wananchi kuendelea kufanya kazi kwa bidii ikiwa ni
ishara ya kumuenzi kiongozi huyo ambaye alikuwa mchapakazi mzuri na
kuwa mfano wa kuigwa.
Comments
Post a Comment