WATENDAJI WA VIJIJI WAKALIA KUTI KAVU. DAS ATAKA FEDHA ZA MAKUSANYO KULESHWA


Uongozi wa Halmashauriya wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa umesema hautasita kuwachukulia hatua kali za kisheria ikiwemo kuwafikisha mahakamani watendaji wote wa vijiji na kata ambao watashindwa kuwasilisha fedha benki za mapato ya ndani na kukaa nazo majumbani kinyume na utaratibu.

Akiongea kupitia mwendelezo wa vikao kazi vilivyofanyika katika tarafa za Ulumi na Mambwenkoswe,Katibu Tawala wilayani humo,Frank Sichalwe, amesema baadhi ya watendaji wamekuwa wakikyuka madili yao ya kazi na kutumia fedha katika matumizi yao binafusi.

‘’acheni mtindo wa kukaa na fedha za makusanyo majumbani mwenu, baada ya  uchaguzi tutaanza kukagua mtendaji mmoja baada ya mwingine na atakae bainka atachukuliwa hatua kali  za kisheria.alisisitiza sichalwe.


Comments