katika picha ni msimamizi msaidi wa uchaguzi jimbo la Kalambo Kanoti Mbawala akiongea na wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya vijiji ,kata na vitongoji. |
Na Baraka Lusajo. Kalambo.
UONGOZI wa Halmashauri ya wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa
umewaonya watendaji pamoja na wasimamizi wa uchaguzi utakao fanyika
kesho kutojihusisha na vitendo vya udanganyifu vinginevyo watachukuliwa hatua
kali za kisheria.
Onyo hilo limetolewa jana na msimamizi msaidizi wa
uchaguzi wa wilayani hiyo Mbawala Kanoti katika kikao kazi kilicho
fanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo.
Alisema kuwa mara kwa mara wasimamizi wa uchaguzi katika vituo
vya kupigia kura ndiyo wamekuwa wakisababisha wananchi kutokuwa na imani na matokeo
kutokana na baadhi yao kukiuka madili yao ya kazi kwa kuchukua hongo
kutoka kwa wagombea.
Alisema kuwa kufanya kazi kinyume taratibu kumekuwa
kukisababisha malalamiko hivyo kuwataka kujiepusha na vitendo hivyo
ili kufanya uchaguzi huo kuwa wa amani.
"uzoefu unaonyesha sisi watendaji wa
serikali ndio tumekuwa vinara kwani tumekuwatu kisababisha kuibuka malalamiko
kutoka kwa wa pigakura ,pia lazima mkumbuke kuwa vyombo vya
sheria havita wavumilia endapo mtakwenda kinyume na utaratibu'’alisema
Alisema kuwa katika uchaguzi huo vitongoji 78,vijiji
33 na kata 14, ndio vitashiriki katika uchaguzi huo.
Msimamizi huyo wa wilaya alisema kuwa katika wilaya hiyo
jumla ya vijiji 78, vitongoji
na kata 344 hakutakuwa na uchaguzi kutokana na wagombea wa
baadhi ya vyama pinziani kujitoa na wengine kuondolewa kutokana
na kuwekewa pingamizi hali inayotoa fursa kwa wagombea wa Chama cha
Mapinduzi kupita bila kupingwa.
katika picha ni baadhi ya wasimamizi wa vituo vya uchaguzi |
Alisema kuwa uchaguzi utaanza majira ya saa
2:00 za asubuhi na kuhitimishwa saa 10:00 za
jioni na aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura
kwa lengo la kuchagua viongozi bora na ambao watakuwa
masaada katika maeneo yao na taifa kwa ujumla.
Kwaupande wao watendaji pamoja na wasimamizi hao walisema kuwa
wamejipanga vizuri ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani
na utulivu na wanaimani kuwa hakutakuwa na malalamiko kwakua taratibu zote
zitafuatwa.
Comments
Post a Comment