Na Baraka Lusajo.
Wakulima wilayani Kalambo mkoani Rukwa wamelalamikia
kukosekana kwa pembejeo pamoja na bei elekezi katika msimu huu wa kilimo
hali inayotia hofu kutopata mavuno kutokana na wakulima wengi kulima bila
kutumia pembejeo.
Mmoja wa wakulima hao Samu Mwasomola, alisema kuwa kumekuwepo na
changamoto ya upatikanaji wa pembejeo za kilimo kitendo kinachopelekea
wakulima kutumia mbegu zisizo faa na zisizo na ubora.
Naye
Edwini Mwasabwite,alisema kuwa wanaiomba serikali kuwa na mazoea ya kuwahisha pembejeo za kilimo kabla ya msimu
kuanza kwa lengo la kuwawezesha wakulima kupata mazao mengi na
kuondokana na adha ya kutumia pembejeo zisizo na ubora.
Naye kaimu
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kalambo Nikoraus Mrango, alisema kuwa
serikali imesambaza pembejeo za kilimo katika maduka
yote yanayouza pembejeo sambamba na kutoa bei elekezi.
Alisema kuwa
kinachofanyika hivi sasa ni kukagua kama pembejeo hizo zinawafikia
wakulima na kuwataka wakulima kutoa taarifa endapo kuna
changamoto zinazowakabili katika maeneo
yao husika.
‘’tutachukua
hatua kali kwa mujibu wa sheria endapo kuna
wauzaji wa pembejeo watakao bainika kukiuka taratibu
wakati wa kuwauzia pembejeo wakulima’’alisema Mrango.
Awali
akiongea kupitia madhimisho ya msimu
wa kilimo Julieth Binyura
aliwataka watendaji wa Halmashauri hiyo kusimamia na kuhakikisha
wauzaji wa pembejeo wanauza pembejeo za kilimo
kwa bei elekezi.
Pia
alisema wilaya inaendelea kusisiza wakulima kulima kibiashara mazao
mbalimbali ikiwemo Alizeti na kahawa ili kuongeza wigo wa mazao
yanalimwa na kupunguza utegemezi kwenye zao la mahindi ambalo
wakati mwingie bei yake imekuwa haitabiliki.
Hivi karibuni
mkoa wa Rukwa ulizindua msimu mpya wa kilimo kwa mwaka 2019/20 na unakusudia kulima hekta
603,637.13 za mazao mbalimbali ili kuhakikisha wananchi wanakuwa na uhakika wa
chakula.
Mwisho
Comments
Post a Comment