RC Wangabo Aviagiza Vyombo Vya Dola Kumsaka Na Kumkamata Mkadarasi Anajenga Barabara Ya Mji Wa Matai.

Katika  picha ni mkuu wa  mkoa  wa Rukwa  Joachm Wangabo.


MKUU wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo ameiagiza tasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) kumsaka na kumkamata mkandarasi wa kampuni ya Grand Tech LTD ya jijini Dar es salaam inayotengeneza barabara ya Lami yenye urefu wa kilometa mbili katika mji wa Matai wilayani Kalambo kwa tuhuma za kulipwa fedha zaidi ya nusu ya kazi kisha kuitelekeza.

Agizo hilo alilitoa jana katika kikao cha bodi ya barabara ya mkoa huo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa huo.
wajumbe  wa kikao

Mkuu huyo wa mkoa ambaye pia ni mwenyekiti wa kikao cha bodi hiyo alitoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa mkuu wa wilaya ya Kalambo Julieth Binyura aliyelalamikia mkandarasi huyo kulipwa fedha kiasi cha shilingi milioni 544.2 sawa na asilimia 67 ya fedha yote ya mradi huo ambayo ni shilingi milioni 899.7 na kisha kuitelekeza kazi hiyo.
 

Alisema kuwa kwa mujibu wa mkataba wa mkandarasi huyo alipaswa kuwa ameisha kamilisha ujenzi wa kipande hicho cha barabara na kufikia Novemba 2 lakini bado na mpaka sasa yupo kwenye muda wa makato kutokana na kuchelewesha kazi hiyo.

Mkuu huyo wa mkoa aliiagiza takukuru kufikia siku ya jumatatu wiki ijayo ni lazima mkandarasi huyo awe amefikishwa mkoani Rukwa kwaajili ya kuhojiwa ili kujua sababu za yeye kutotelekeza kazi hiyo pamoja na mchakato wa kumlipa fedha zote  hizo wakati kazi hiyo haina thamani ya kulipwa fedha hizo.

Kwaupande wake mkuu wa Takukuru mkoa wa Rukwa Hamza Mwenda aliahidi kutekeleza agizo hilo ili kuwaondolea kero wananchi wa mji wa Matai ambao wamekuwa wakilalamikia kipande hicho cha barabara kwakuwa kimekuwa kero kwakua ndicho kinacho chepuka na kuingia makao makuu ya wilaya hiyo kutoka katika barabara kuu ya kutoka Sumbawanga mjini kwenda katika bandari ya Kasanga.


Comments

  1. Kweli inachosha sana, matai ni Mji ulio na wakazi wengi, pia wageni wanao ingia na kutoka ni wengi. Barbara hiyo itaongeza chachu kwa wananchi na wageni wanao ingia na kutoka.

    ReplyDelete

Post a Comment