Makasisi wa kikatoliki wafungwa jela kwa kuwanyanyasa watoto viziwi Argentina.
on
Get link
Facebook
Twitter
Pinterest
Email
Other Apps
Nicola Corradi (kulia- katika kiti cha walemavuin na Armando Gómez (katikati) na Horacio Corbacho (kushoto) wakiondoka mahakamani mjini Mendoza
Mahakama nchini Argentina imewahukumu makasisi wawili wa Kanisa
Katoliki la Roma kifungo cha zaidi ya miaka 40 jela kila mmoja kwa kuwanyanyasa
kingono watoto viziwi katika shule ya kanisa.
Horacio
Corbacho na Nicola Corradi, pamoja na muhudumu wa bustani, walipatikana na
hatia ya kuwabaka na unyanyasaji katika shule ya kikatoliki iliyopo katika
jimbo la Mendoza kuanzia mwaka 2004 hadi 2016.
Waathiriwa
kadhaa walikuwa mahakamani kushuhudia kutolewa kwa hukumu Jumatatu.
Kesi
hiyo imeishitua Argentina, nchi ambayo anatoka Papa Francis, huku wengi wakilishutumu
kanisa kwa kuzorota kuchukua hatua.
Kanisa
Katoliki limekabiliwa na shutuma za unyanyasaji wa kingono wa watoto katka
maeneo mbali bali duniani katka kipindi cha miongo michache iliyopita.
Mahakama ilibaini nini?
Jumatatu,
mahakama katika mji wa Mendoza alimhukumu kasisi wa Kiargentina kifungo cha
miaka 45 jela.
Comments
Post a Comment