Pembejeo kuwafikia wakulima kwa wakati mkoani Rukwa



Katikati ni mkuu  wa  wilaya  ya  Kalambo  Julieth Binyura akikagua  bidhaa mbalimbali.
Mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote za mkoa huo kusimamia kwa karibu uingizwaji wa pembejeo za kilimo na kuhakikisha zinauzwa kwa bei elekezi ili kuwafikia wakulima kwa muda muafaka.

Akiongea kupitia madhimisho ya ufunguzi wa msimu mpya wa kilimo kwa mwaka  2019/2020 Wilayani Kalambo,Mkuu wa Mkoa wa Rukwa aliyewakilishwa na Mkuu  wa Wilaya ya Kalambo Julieth Binyura,amesema katika kipindi cha mwaka 2019/2020 mkoa unalenga kulima jumla ya hekta 603,637.5 za mazao  mbalimbali.

‘’kati ya hizo hekta 524,800.7 ni za mazao ya  chakula ,hekita 76,363.08 za mazao ya biashara na hekta 2,473.35 za mazao mbalimbali ya mbogamboga na matunda. ‘’alisema Binyura .

Alisema jumla ya tani 1,731,495.5 za mazao zinategemewa  kuzalishwa  ambapo  kati ya  kiasi  hicho tani 1,602,5201.1 ni za  mazao ya chakula ,tani 115,800 za mazao  ya mbogamboga na matunda.
‘’nitoe  maelekezo  kwa  watendaji wote wa  Halmashauri zote kuhakikisha mbolea hizi zinauzwa kwa bei elekezi na zinawafikia wakulima katika maeneo  yote’’alisema Binyura.
Mwakilishi wa tasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Briten, Progers Mbugi,amesema mpaka sasa wameweza kufikia wakulima 54,000 kwa kuwapatia elimu na misaada  mbalimbali.
‘’mpaka sasa kupitia mradi huu tumeweza kuwafikia zaidi ya wakulima wadogo wadogo 54,000 wake  kwa  waume ,kutoka katika vyama vya msingi  vya ushirika vya mazao –AMCOS  pamoja  na wale walio nje ya vyama hivi. Lengo letu hadi  kufikia mwisho wa mradi huu 2020 tuwe tume wafikia wakulima 72,000.’’Alisema Progers Mbugi.
Kwa upande wa wakulima wilayani humo wameiomba serikali  kutoa pembejeo za kilimo mapema kabla ya  msimu kuanza.




Comments