Uongozi wa serikali
wilayani Kalambo mkoa
wa Rukwa umeanzisha
utaratibu wa kuwatambua wastaafu wa utumishi wa umma ili kuwasaidia kupata haki
zao na kujua taarifa za utumishi wao kwa ajili ya mahitaji ya lazima
yanayojitokeza kwenye ofisi za umma wilayani hapa siku hadi siku.
Katibu tawala wa
wilaya ya Kalambo, Frank Sichalwe, amesema
kikao cha kwanza cha kuchagua viongozi wa umoja wa wastaafu wa utumishi wa umma
wilayani humo kimebaini dosari za kiutendaji zinazokwamisha upatikanaji wa
haki na stahiki zao kwa wakati.
Aidha ameelezea
umuhimu wa kuunda umoja wa wastaafu wa utumishi wa umma kwa ajili ya kutatua
changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika maisha yao mara baada ya kukoma
muda wa utumishi wa umma.
Wakitoa hisia zao kupitia
kikao kilicho jumuisha watumishi wastaafu wilayani Kalambo wameelezea jinsi wanavyokabiliwa na changamoto ya
kupata haki na stahili zao ikiwa ni pamoja na kukabiliwa na vitendo vya kuombwa
rushwa au kutapeliwa haki na stahili zao.
‘’tunaimani umoja huu
utatusaidia kuondokana na vitendo vya utapeli kwani baadhi yetu tumetapeliwa mara kadhaa na
kuupongeza uongozi wa wilaya hiyo
kwa kuunga mkono juhudi zao’’.Walisema wastaafu hao.
Afisa utumishi wa
Halmashauri ya wilaya ya Kalambo Amandus Mtani amewataka wastaafu wote kufika
kwenye ofisi yake pindi kunapotokea changamoto yoyote kwa
lengo la kuitatua
kwa wakati.
‘’kimsingi wazee ni
hazina ya jamii yoyote duniani na kwamba ni kundi muhimu linalo beba tunu na
utamaduni uliotukuka kwa ajili ya maendeleo ya nchi hususani tanzania. hivyo Halmashauri
itaendelea kutoa huduma kwa jamii na watumishi wote wakiwamo
wasitaafu.’’alisema Amandus Mtani.
Comments
Post a Comment