Ameyasema
hayo kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata
ya Matai Wilayani Kalambo
mkoani Rukwa, ambapo amesema jeshi la Polisi liko imara na linafanya kazi usiku na mchana hivyo
haliwezi kushindwa kuwakamata wabakaji
wanaokimbilia kwenye nchi jirani ya Zambia
na kokote kule baada ya
kufanya uhalifu.
‘’Watoto
hawa lazima walindwe, wabakaji hawawezi kulishinda jeshi la Polisi. Natoa siku
saba wote wawe wameishakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria na taarifa
hiyo niipate haraka.’’Amesema lugola huku akishangiliwa na mamia ya wananchi.
Aidha,
amewataka maredeva wa magari na bodaboda kufuata sheria za usalama barabarani
hususani wakati wa kuendesha vyombo vya moto. Vinginevyo watachukuliwa hatua za
kisheria ikiwa pamoja na kunyang’anywa leseni.
Wananchi
kwa upande wao, wameiomba serikali kufungua kituo cha zima moto kwa lengo la
kurahisha upatikanaji wa huduma hiyo pindi majanga ya moto yanapotokea. Hivi
sasa huduma hiyo inapatikana Manispaa ya Sumbawanga umbali takribani kilometa
52, kutoka Mji wa Matai ambao ndio makao makuu ya Wilaya ya Kalambo.
Aidha
wamempongeza mkuu
wa wilaya ya kalambo Julieth Binyura pamoja
na uongozi wa Halmashauri hiyo kwa kusimamia shuguli mbalimbali za
maendeleo ikiwemo ujenzi
wa vituo vya afya pamoja
na hospital ya wilaya.
‘’kusema
kweli mmetuletea mkuu wa wilaya ambae ni mchapa kazi kwani japo kuwa ni mama lakini
anachapa kazi kama mwanaume’’walisema wananchi hao.
Comments
Post a Comment