Na Ezekiel Kamanga. Mbeya .
Watu watano mkoani Mbeya akiwemo
Mfanyabiashara ya madini wilayani Chunya Sauli Mwalabila wamefikishwa
mahakamani kwa tuhuma za uhujumu uchumi katika shughuli za madini.
Pia mshtakiwa wa pili Sauli Samson
amechukuliwa na jeshi la polisi mkoani Mbeya baada ya mahakama ya hakimu mkazi
Mbeya kukubali maombi ya serikali kumchukua mtu huyo kwa mahojiano juu ya kesi
ya uhujumu uchumi anayoshtakiwa nayo pamoja na wenzake wanne mkoani humo.
Mwendesha mashtaka wa serikali
wakili mwandamizi Basilius Namkambe akisoma shkata hilo la uhujumu uchumi namba
23/2019 amewataja washtakiwa kuwa ni Micky Konga (53) mkazi wa majengo Itewe na
mwenzake Sauli Solomon Mwalabila (39) mkazi wa kiwanja wilayani Chunya.
Amesema wawili hao wanashtakiwa kwa
makosa mawili ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kinyume na kifungu
namba 302 na 337 ambapo kati ya juni mosi 2019 na Julai 30, 2019 jijini Mbeya
walijipatia dola za kimarekani laki moja na 15 kwa ajili ya ununuzi wa madini
aina ya dhahabu kutoka kwa raia wa kigeni kutoka nchini Ujerumani Henry Clemar
kiasi cha kilo moja wakati sio sahihi kosa la pili likiwa ni uhujumu uchumi
kinyume na kifungu namba 12 (b) na 13 (a).
Baada ya Jamuhuri kueleza hayo
wakili wa upande wa utetezi Baraka Mbwilo aliitaka mahakama kuzuia mteja wake
kutochukuliwa na maaskari hao akisema tangu mfanyabiashara huyo akamatwe
sept.mosi mwaka huu alikuwa mikononi mwa polisi waliomsafirisha hadi Dar es
Salaam hadi jumatatu hii laasivyo wakaombe magereza kuendelea na uchunguzi wao
na kuiomba mahakama iruhusu gari la mshtakiwa lirejeshwe kwa ndugu zake akidai
haihusiani na kesi hiyo.
Akijibu hoja hiyo ya utetezi wakili
Namkambe wa serikali amesema gari hilo haliwezi kuruhusiwa kwakuwa ni sehemu ya
ushahidi maombi na ambayo yameungwa mkono na mahakama kupitia hakimu Denis
Luwungo hata kuamuru baada ya kesi hiyo mshtakiwa achukuliwe na jeshi la polisi
kwa upelelezi zaidi juu ya shauri hilo.
Pia washtakiwa hao mwingine Emmanuel
Kessy Joachim (35) mkazi wa Uyole Mbeya wamefikishwa katika mahakama ya hakimu
mkazi Mbeya Andrew Scout na kusomewa pia mashtaka mengine mawili ya kujipatia
fedha kwa njia ya udanganyifu na utakatishaji fedha kutoka kwa Sevia Matope
raia wa nchini Zambia kiasi cha kwacha 290.
Pia washtakiwa wengine wawili
Eveline Bahati (22) mfanyabiashara na na Tyson Jeremia (25) mkulima wote wakazi
wa kibaoni chukaa wilayani Chunya wamefikishwa mahakamani Mbeya wakituhumiwa
kwa makosa matatu ya kupanga uhalifu, kupatikana na madini sanjari na
utakatidhaji wa fedha kosa walilolifanya katika tarehe tofauti kati ya Juni
mosi na Agosti 30 mwaka huu huko wilayani Chunya ambapo baada ya kusomewa
mashtaka hayo hakimu mkazi katika mahakama ya hakimu mkazi Mbeya Happines Albert
Chua ameahirisha shtaka hilo namba 25 la mwaka 2019 hadi Septemba 23 mwaka huu.
Katika kesi na makosa hayo yote
washtakiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kutokana mahakama hizo kutokuwa na
mamlaka kisheria kusikiliza mashauri hayo ya uhujumu uchumi isipokuwa mahakama
kuu ya Tanzania au mahakama ya chini kwa kibali cha mahakama kuu.
Naibu waziri wa madini yupo mkoani
Mbeya kwa ziara ya kikazi anasema serikali haitamfumbia macho mchimbaji au
mfanyabiashara wa madini atakayekuwa akifanya shughuli hizo kinyume cha sheria
ya madini na kuiingizia hasara serikali ambayo inajitahidi kujenga masoko ya
madini ili kuisaidia jamii nzima ya watanzania.
Comments
Post a Comment