katika picha ni msimamizi wa uchaguzi wilayani kalambo akiongea na wanahabari ofisini kwake. |
Na Baraka Lusajo. Kalambo.
Zikiwa
zimesalia siku chache kuanza kwa uchaguzi mkuu wa serikali za mitaa hapa nchini
,wananchi wilayani Kalambo mkoani Rukwa wameiomba serikali kuthibiti mianya ya wahamiaji haramu kuingia nchini kinyemera sambamba
na kuongeza vituo vya kupigia kura pamoja na kuweka utaratibu maalmu kwa wazee na
watu wasio jiweza ili kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo.
Jumla
ya wananchi lakimoja kumi na nne elfu mia tisa hamsini na moja (114,951)
wanategemea kuanza kupiga kura za kuwachagua viongozi wa serikali za vitongoji
na vijiji ifikapo November 24,2019, ambapo kwa wilaya ya Kalambo zoezi hilo
litafanyaka kwenye vijiji mia moja kumi
na moja(111) katika vituo mia nne ishirini na mbili(422).
Kufuatia
umuhimu wa zoezi hilo wananchi wilayani humo wametoa maoni yao na huku wengi
wao wakiomba serikali kuweka utaratibu mzuri ambao utasaidia akina mama
wajawazito, wazee pamoja na watu wenye hali ya ulemavu kuweza kupiga kura kwa
urahisi zaidi na kuchagua kiongozi wanae
mtaka.
‘’tunaomba
serikali kuongeza vituo vya kupigia kura pamoja na kuweka utaratibu maalumu
ambao utasaidia wazee pamoja na watu wenye hali ya ulemavu kupata huduma kwa urahisi
zaidi kwa kuawachagua viongozi wanaotaka bila bugudha’’walisema wananchi hao.
Msimamizi
mkuu wa uchaguzi wlayani humo Eriki Kayombo,amesema vituo vya kupigia kura
vitafunguliwa kuanzia majira ya saambili asubuhi hadi saa kumi na moja jioni na
kuwasihi wananchi kujitokeza kwa wingi
kuchagua viongozi wanao wataka kwa masirahi mapana ya taifa.
‘’kura ni haki yako,kumbuka
kupiga kura tarehe 24 november 2019 ili upate kiongozi bora atakae kuletea
maendeleo na vituo vya uandikishaji vitafunguliwa kuanzia 2:00 asubuhi na
kufungwa saa 12:00 jioni na vituo vya kupigia kura vitafunguliwa kuanzia saa2:00
asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni.’’alisema Kayombo.
Afisa
uchaguzi wilayani humo Atanas Saida,amesema wamegawa vitendea kazi mbalimbali
kwa wananchi, mashirika ya dini pamoja
na watu wengine.
‘’kusema
kweli tumejipanga vizuri na mpaka sasa tumekwisha kugawa vifaa mbalimbali kwa
mashirika ya dini watu maalufu, pamoja
na watumishi’’.alisema Saida.
Hata
hivyo serikali wilayani humo imetangaza nafasi mianne ishirini na mbili za kazi
ya uandikishaji na uandaaji wa orodha ya
wapiga kura ,zoezi ambalo litamudu kwa
muda wa
siku saba.
Comments
Post a Comment