Wahudumu Wa Afya Washumiwa Kuendekeza Vitendo Vya Utoro Makazini.

katika picha ni mkuu  wa wilaya  ya  Kalambo Julieth Binyura 


Na Baraka Lusajo.Kalambo.

Mkuu wa wilaya ya kalambo Julieth Binyura amemwagiza mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Msongela Palela kufuatilia na kuwachukulia hatua kali za kinidhamu wahudumu wa afya ambao wamekuwa wakitoroka muda wa kazi kwenye vituo vyao na kupelekea malalamiko kutoka kwa wagonjwa kutokana na kukosa huduma kwa muda unaostahili.

Ameyasema hayo wakati akisikiliza kero mbalimbali za wananchi kupitia mkutano wa hadhara uliojumuisha vijiji nane kutoka kata za Lyowa na Matai wilayani kalambo mkoani hapa na kuwasisitiza wahudumu wa afya kufanya kazi  kwa bidii na kuondokana na vitendo vya utoro  kwenye  maeoneo yao ya kazi kwa  lengo la  kuondokana na malalamiko yasiyo kuwa ya lazima kutoka kwa wananchi.

‘‘Hili nalikemea lisitokee tena na sasa naanzisha utaratibu wa kukagua nyakati za usiku na ambaye nitakuta hayupo nitamchukulia hatua kwani atakuwa amevunja  sheria.’’ Alisema Binyura.
katika picha ni kaimu mkurugenzi  Efraim Moses 

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri hiyo Efraim Moses Mwalemba amewataka  madiwani kushirikiana na watendaji wa kata na vijiji katika kukusanya mapato ambayo yatasaidia kuendeleza shughuli za maendeleo.

‘’Waheshimiwa madiwani ndio wenye jukumu la kukusanya mapato wakishirikiana na  watendaji  wa vijiji na kata kwenye maeneo yao husika kwani fedha hizi huwa  zinatumika  katika  shughuli mbalimbali za serikali ikiwemo  kuendeleza miradi ya Serikali, kulipa posho za madiwani na mambo mengine yahusuyo usitawi wa Halmashauri.’’alisema Moses

Comments