katika picha ni baadhi ya watumishi wamipewa elimu juu ya umuhimu wa zoez laa upigaji kura |
Haki,usawa
na wajibu vimetajwa kuwa nyenzo muhimu katika makuzi na mwendelezo wa amani kwa
maendeleo ya Wilaya ya Kalambo, Tanzania na bara la Afrika kwa ujumla.
Akiongea
katika kikao cha wadau wa uchaguzi kilicho wajumuisha viongozi, mila Taasisi na
watu maarufu Wilayani Kalambo,Msimamizi wa uchaguzi Wilaya ya Kalambo Erick
John Kayombo, amesema wadau hao wana wajibu wa kushirikiana na Serikali
kuelimisha Wananchi juu ya umuhimu wa kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa
unaotarajiwa kufanyika Kitaifa Tarehe
24/11/2019 kwa ari na mshikamano kwa kuzingatia haki na usawa ili
kuendeleza amani na umoja wa Kitaifa.
Wilaya
ya Kalambo inayokadiliwa kuwa na jumla ya watu 271,393 wakiwemo wanaume 131,285
na wanawake 140,108 ambao wote wanatakiwa kuhamasishwa vilivyo ili washiriki
uchaguzi wa Serikali za mitaa tarehe 24/11/.2019,Ina jumla ya vitongoji
422,Vijiji 111 kata 23 na tarafa 4.ikiwemo Matai,Kasanga,Mwimbi na tarafa ya
Mambwe inayopakana na nchi jirani ya Zambia kwa upande wa Kasikazini pamoja na
Wilaya ya Momba upande wa kusini Mashariki.
Msimamizi
wa uchaguzi Wilaya ya Kalambo Erick John Kayombo, amesisitiza kuwa maendeleo
hayawezi kuja kama Jamii haitakuwa na uongozi bora,
“Nadharia
za kale za wanafalsafa kama vile Cara Max na John Luke zinamwelezea mwanadamu
kuwa ni mnyama wa kisiasa anayehitaji kuongoza na kuongozwa ili pawepo na amani
na kujihakikishia maendeleo ya kweli katika jamii.
‘’
tukiwa wadau wa uchaguzi Wilayani Kalambo tunawajibu wa kuihamasisha jamii
kujitokeza kuandikishwa kwenye daftari la wapiga kura na kuchukua fomu za
kugombea nyadhifa mbali mbali kam vile uenyekiti wa vijiji na vitongoji pamoja
na ujumbe wa Serikali za vijiji ifikapo tarehe 29/10/2019.’’ Anafafanua Erick
Kayombo.
Comments
Post a Comment