Na mwandishi wetu.Sumbawanga.
Mkutano mkuu wa chama cha wafanyakazi wa serikali za mitaa-TALGWU- mkoa
wa Rukwa umewaagiza
makatibu wa halmashauri zote nne za mkoa huo kutumia msaada wa kisheria ili
kuwathibiti badhi ya waajiri wanaotuhumiwa kudhulumu haki na stahili za
wafanyakazi wao.
katibu wa TALGWU mkoa wa Rukwa, Sospeter Challo amezitaja
baadhi ya haki na stahili wanazodhulumiwa wafanyakazi katika halmashauri
za wilaya ya Sumbawanga, Nkasi,
Kalambo na manispaa kuwa
ni pamoja na kunyimwa masurufu ya uhamisho na kuelezea moja ya maazimio ya mkutano mkuu wa chama hicho
katika kuthibiti haki za watumishi wanapopata uhamisho haki zinazodaiwa
kuminywa na baadhi ya waajiri.
Mgeni rasmi katika mkutano huo wa TALGWU ngazi
ya mkoa mkuu wa wilaya ya Sumbawanga dokta Halfany Haule ,amesema baadhi ya
watumishi katika serikali za mitaa wanatuhumiwa kushindwa kutimiza wajibu wao
kwa ajili ya kutaka kujinufaisha wenywewe.
mkutano mkuu wa siku mbili wa wajumbe wa mkutano mkuu wa chama
cha wafanyakazi wa serikali za mitaa-TALGWU-mkoa wa Rukwa umehusisha
pia mafunzo ya uelewa wa sheria mahali pa kazi
Comments
Post a Comment