Na Baraka lusajo. Kalambo.
katika picha ni madiwani wilayani kalambo |
Mkutano
wa baraza la madiwani katika halmashauri ya wilaya ya kalambo mkoani Rukwa
umewapiga marufuku wafanyabishara wote kusafirisha mizigo ya mazao nyakati za
usiku ikiwa ni jitihada za kudhibiti upotevu wa fedha za mapato na kumtaka mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Msongera paela,
kuhakikisha anaweka migambo kwenye mageti yote sambamba na kuweka utaratibu
mzuri wa kukusanya fedha kutoka kwa watendaji wa vijiji.
Halmashauri
ya wilaya ya kalambo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2018/2019 ilikuwa na
makisio ya kukusanya
fedha kupitia vyanzo vyake
vya ndani kiasi cha shilingi bilion
mbili na kufanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi bilioni moja nukuta mbili sawa na asilimia 61.05.
Awali
wakiongea kupitia kikao cha baraza la madiwani wilayani humo, wamesema kwa mwaka
2019 na 2020 wameazimia kufikia malengo ya ukusanyaji mapato kwa kushirikina na watendaji wa vijiji na kata na kumshauri mkurugenzi
mtendaji kutowaruhusu watendaji kukaa na fedha za makusanyo kwa muda mrefu.
mkurugezi mtendaji wilayani kalambo |
Mkurugezi
mtendaji wa halmashauri hiyo Msongera
palela ,amesema wamejipanga kubuni vyanzo vipya vya mapato nakuwasihi
madiwani kutoa ushirikiano katika zoezi zima la ukusanyaji mapato.
‘’Tumejidhatiti
kuanzisha zoezi la kutoa hati za ardhi za kimila na leseni za makazi kwa
wananchi pamoja na kutoa elimu juu ya manufaa ya mpango huo ili Halmashauri
ipige hatua mbele’’alisema msongela.
Katibu
tawala wilayani humo Frank Sichalwe, amesema ofisi ya mkuu wa wilaya itaendelea
kuwasaka na kuwachukulia hatua watendaji wote ambao washindwa kufanya marejesho ya fedha za mapato kwa muda muafaka.
‘’ofisi
ya mkuu wa wilaya kwa kushirikiana na ofisi ya mkurugezni mtendaji wa halmashauri
itaendelea kuwasaka na kuwachukulia
hatua waatendaji ambao
wagundulika kukaa na fedha majumbani kama ilivyo fanya kwa
mwaka wa fedha uliopita’’ alisema sichalwe.
Comments
Post a Comment