Na Baraka Lusajo. Kalambo.
Halmashauri ya wilaya
ya kalambo mkoani Rukwa imefanikiwa kuongeza
kiwango cha ukusanyaji wa mapato ya serikali kutoka zaidi ya shilingi milioni
mia nane kwa mwaka wa fedha 2017/18 hadi
zaidi ya shs bilioni moja kwa mwaka wa fedha 2018/19 kutokana na kuziba mianya ya matumizi yasiyokuwa
sahihi ya fedha.
Kaimu mweka hazina wa Halmashauri
ya wilaya ya Kalambo,Agustino Manda amewaeleza
wajumbe wa kikao maalumu cha baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo kilichoketi
kuridhia mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha ulioishia june 30 kuwa uadilifu
mahali pa kazi umewezesha mafanikio hayo.
Aidha ameelezea jinsi
watumishi wa umma katika Halmashauri hiyo walivyozingatia njia sahihi za mapato
na matumizi kwa mujibu wa sheria na kwa
kuzingatia nidhamu ya matumizi bora ya fedha za serikali ‘’Financial memorandum of
2017.’’
Mwenyekiti wa
Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo,
Daudi Sichone, amesema ushirikiano wa pamoja kati ya wataalamu na
viongozi wa kisiasa kwa maana ya madiwani umewezesha kuongezeka kwa mapato ya
Halmashauri kunakozingatia kanuni taratibu na sheria ya fedha.
Kaimu Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo,
Ephraim Mozes pamoja na baadhi
ya madiwani Wilayani humo
hawakusita kuelezea mikakati
ya Halmashauri hiyo katika
swala zima la
ukusanyaji mapato na kusema.
‘’tumenzisha oparesheni ya kukagua magari nyakati za usiku hususani yale
ambayo yanahusika na ubebaji wa mazao ya
nafaka kwani baadhi
ya madereva wamekuwa
wakitorosha mizigo bila
kulipa ushuru’’ walisema
viongozi hao.
Imeelezwa kuwa
mikakati bora ya usimamaizi wa mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo umewezesha kuongezeka asilimia ya ukusanyaji
kutoka asilimia 47 hadi kufikia asilimia 61 na hivyo kuwa na uwezo wa
kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.
Comments
Post a Comment