Katika picha ni mkurugezi mtendaji kalambo. |
Na Baraka Lusajo- Kalambo.
Mkurugenzi
mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa Msongela Palela
amezitaka kamati zote zinazohusika na maswala ya ukatili wa kijinsia
kushirikiana na viongozi wa serikali za vijiji na kata katika kutokomeza mila
potofu zilizojengeka katika jamii na kuwaagiza maafiasa maendeleo ya jamii
kufuatilia na kutoa ripoti sahihi juu ya utekelezaji wa kazi hizo.
Ameyasema
hayo wakati wa uzinduzi wa kamati za kupinga ukatili na mila potofu wilayani Kalambo
mkoani hapa,ambapo amesema lengo la serikali ni kuhakikisha ukatili wa kijinsia
na mila potofu zinatokomezwa katika jamii kwa kutoa elimu sitahiki kwa wananchi.
Amesema
kamati hizo zitafanyakazi katika kata ishirini na tatu za wilaya hiyo na kuzitaka kamati
hizo kuhakikisha elimu waliopatiwa
inawafikia wananchi wote kwa muda muafaka.
‘’yale
malengo tuliojiwekea ndio tukayatekeleze na mtakapo rudi katika
vijiji na kata zenu nendeni mkawe
walimu wazuri kwani hivi leo mmefundishwa ili mkawafundishe wengine’’.alisema Msongela.
katika picha ni mwezeshaji wa mafunzo, Faustina Valeli |
Mwezeshaji
wa mafunzo hayo Faustina Valeli amezitaka kamati hizo kufichua matukio ya ukatili
wa kijinsia sambamba na kuwachukulia hatua kali wahusika wa matukio hayo kwa
kuwafikisha kwenye vyombo vya dora kwa hatua zaidi za kisheria.
katika picha ni mkurugenzi wa asasi yaSucoda. |
Mkurugezi
kutoka Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya Sukoda Samweli Mwazunga,amesema mradi
huo utajikita zaidi katika kutoa elimu kwa jamii juu na namna
ya kuepuka ukatili wa kujinsia na
Mila potofu katika jamii.
Mafunzo
hayo yameshirikisha walimu wa shule za msingi na sekondari, Wahudumu wa afya
vijijini (WAVI) , maafisa maendeleo
ya jamii pamoja na watendaji .
mawasiliano zaidi. 0762432747.
Comments
Post a Comment